BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, December 06, 2011

KILIMANJARO STARS NA UGANDA CRANES ZAINGIA NUSU FAINALI

Timu ya Kilimanjaro stars na Uganda Cranes zimefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali ya kombe la Tusker chalenji 2011,Uganda wamepata nafasi hiyo kwa kuwafunga Zimbabwe bao 1-0 kwenye mchezo uliochezwa mchana uwanja wa taifa.
 Mchezo mwingine uliwakutanisha mabingwa watetezi Kilimanjaro Stars na timu ya taifa ya Malawi na matokeo ni Kilimanjaro Stars wameibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na kiungo Nurdin Bakar kwa shuti kali na hivyo matokeo kubaki hivyo hadi mwisho wa mchezo.

No comments:

Post a Comment