BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, August 28, 2011

Manchester yaifanyia kufuru Arsenal yawachapa 8-2


Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Uingereza leo wameifanyia kitu mbaya timu ya Arsenal kwa kuichapa mabao 8-2,kichapo hicho ni kikubwa kwa maisha ya mzee Arsenal Wenger ambaye ana tabia ya kujiamini sana,na sasa amekuwa na wakati mgumu kubaki kwenye timu hiyo ambayo amekuwa nayo kwa muda mrefu na inasemekana ndiye kocha pekee aliyeleta mabadiliko kwenye ligi hiyo ya Uingereza na kufuta ubaguzi wa rangi.
Lakini kutokana na kipigo cha leo kinamuweka kwenye wakati mgumu zaidi hasa baada ya kuwauza wachezaji wake nyota na kushindwa kutafuta mbadala wao,pamoja na bodi ya klabu hiyo kuruhusu fedha zitumike kwenye usajili wa msimu huu lakini alikaidi agizo hili.
Mechi hii imehudhuriwa na watazamaji 73414 kwenye dimba la Old Trafford na Man U kuibuka na ushindi mnono wa bao 8-2.

No comments:

Post a Comment