BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Monday, August 29, 2011

Sir Alex Ferguson amshauri Wenger kufanya usajili makini kabla ya kesho kutwa.


Baada ya Manchester United kuibuka na ushindi wa mabao 8-2 dhidi ya Arsenal,meneja wa Man Utd amemshauri kocha wa Arsenal kufanya usajili makini kwa masaa 48 yaliyobaki kabla ya msimu wa usajili kufungwa hapo jumatano.
Naye Wenger amesema sababu ya kipigo hicho ni uchovu wa wachezaji wake ambao jumatano iliyopita walicheza na Udinesse ya Italia kwenye ligi ya mabingwa Ulaya na hivyo kusababisha majeruhi kwenye kikosi hicho na kufanya wachezaji tisa wa kikosi cha kwanza kutocheza.
Wenger ni kocha pekee aliyeiletea mafanikio timu ya Arsenal na kuifanya kuwa na wapenzi wengi duniani lakini mambo sasa yanataka kumuendea kombo kutokana na kipigo hicho kikubwa ambacho kwa mara ya mwisho timu hiyo ilifungwa mabao 8-0 mwaka 1896,hata hivyo Wenger amewaomba radhi wapenzi na mashabiki wa timu hiyo duniani kote.

No comments:

Post a Comment