BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, July 12, 2011

AIRTEL YAWA KAMPUNI YA KWANZA KUWAFIKIA WANANCHI WA MGAZINI-RUVUMA


Kampuni ya simu za mikononi ya Airtel imezindua mnara wake eneo la Mgazini mkoani Ruvuma,na hivyo kuwaondolea adha ya mawasiliano wakazi wa eneo hilo na maeneo ya Mhepai na vijiji jirani,kiongozi wa Airtel bwana Cheikh Sarr amesema ndani ya mwezi huu wanatarajia kuzindua minara 50 hapa nchini,nilifanikiwa kuongea na mmoja wa wananchi wa eneo la Mhepai bw.Morris Mapunda alionyesha kufurahia huduma hiyo na kudai walikuwa na simu kama mapambo kutokana na kutokuwepo mtandao wowote na ameishukuru sana Airtel kwa kuwaletea huduma hiyo.

No comments:

Post a Comment