BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, July 09, 2011

YANGA YACHAFUA HALI YA HEWA MSIMBAZI

Mabingwa wa Tanzania bara Yanga jana walifanikiwa kuingia fainali ya michuano ya Kagame Cup baada kuwatoa St.George ya Ethiopia kwa mikwaju ya penati 5-4 na hivyo kukutana na Simba kwenye fainali kesho kwenye uwanja wa taifa,Simba ambayo ilionekana kucheza kandanda safi toka ilipoanza michuano hii tofauti na watani wao,watalazimika kucheza kivingine zaidi kutokana na timu kukamiana kila zinapokutana na kuharibu ladha ya mchezo

Mashabiki wa Yanga wakishangilia mara baada ya mpira kumalizika wengine hawakuamini kilichotokea baada ya penati ya mwisho ya St.George kugonga mwamba na kurudi chini jirani na mstari wa goli

No comments:

Post a Comment