BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, May 15, 2011

AJALI


Gari kubwa aina ya scania likiwa limeacha njia na kujikita kwenye mitaro iliyopo pembeni ya barabara,eneo la Iwambi Mbeya.

Msongamano huu umesababishwa na lori liliacha njia na kujikita kwenye mtaro wa barabara eneo la Iwambi-Mbeya.

Thursday, May 12, 2011

MAMA NA MWANA

Mama Mchungaji wa kanisa la moravian usharika wa NZOVWE  mama Salome Kalengo,akiwa na watoto wake walipotembelea ofisini kwake

Sunday, May 08, 2011

MANCHESTER UTD YAICHAPA CHELSEA 2-0


Manchester utd imezidi kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa England baada ya kuwachapa Chelsea kwa bao 2-0,na hivyo kuwa mbele kwa pointi 6 na zikiwa zimebakiwa na mechi 2 nao Arsenal wamepokea kichapo cha bao 3-1 kutoka kwa Stoke City.

KOMBE LA TAIFA


Timu ya mkoa wa Rukwa imeweza kufanya maajabu kwa kuifunga timu ya mkoa wa Temeke kwa jumla ya bao 2-1,Rukwa walikuwa wa kwanza kupata goli kwa njia ya adhabu dakika 12 baadaye nao Temeke walisawazisha nao kwa njia ya adhabu,kipindi cha pili Rukwa walifanikiwa kupata bao la pili.Katika mchezo wa kwanza Mbeya walifanikiwa kuwafunga Iringa 2-1.

Thursday, May 05, 2011

WEMBLEY PATACHIMBIKA


Kocha wa manchester akishangilia ushindi dhidi ya Schalke 04 ya Ujerumani

MANCHESTER UTD USO KWA USO NA BARCELONA MEI 28

Wachezaji wa manchester united wakishangilia moja ya mabao waliopata jana kwenye mchezo wa klabu bingwa ulaya kati yake na SCHALKE 04,ambapo manchester walifanikiwa kupata ushindi wa mabao 4-1 na kusonga kwa jumla mabao 6-1,sasa watakutana na Barcelona katika mchezo wa fainali tarehe 28 mei,kwenye uwanja wa Wembley  England.

Wednesday, May 04, 2011

BARCELONA YATINGA FAINALI

Timu ya Barcelona jana ilifanikiwa kuingia fainali ya klabu bingwa ulaya baada ya kutoka sare na Real madrid 1-1,ilikuwa ni Barcelona iliyokuwa ya kwanza kujipatia lililofungwa Pedro dakika ya 56 madrid walisawazisha dakika ya 66 kupitia Marcus kwa matokeo hayo Barca wanaingia fainali na moja kati ya itakayoshinda leo kati Man utd v/s Schalke 04

SEHEMU ALIYOKUWA AKIISHI OSAMA BIN LADEN

Hii ndio nyumba aliyokuwa akiishi Osama bin Laden eneo la obbottabad nje kidogo ya jiji Islamabad Pakistan,ambayo ilishambuliwa na majasusi wa kimarekani na kufanikiwa kumuuwa kiongozi huyo wa kundi la al quaider

Monday, May 02, 2011

OSAMA BIN LADEN AUAWA PAKISTAN

Kiongozi wa kundi la al-queida ameuawa na wanajeshi wa Marekani waliokuwa wakifanya operesheni maalum nchini Pakistan,Osama bin laden amekuwa akisakwa kwa zaidi ya miaka kumi na moja sasa

Thursday, April 28, 2011

CHANGIA DAMU OKOA MAISHA


Waelimishaji kutoka kitengo cha taifa cha damu salama kanda ya nyanda za kusini,wakitoa elimu juu ya uchangiaji damu kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lwati wilayani Mbozi-Mbeya.Kwa kutumia blog hii nawapongeza wafanyakazi wa kitengo husika na wale wote wenye moyo wa kujitolea kwa ajili ya wahitaji-Amen.

ELIMU NA KAZI


Wanafunzi wa shule ya sekondari Lwati wilayani Mbozi,wakiwa kwenye shamba la migomba wakifanya kazi kwenye moja ya mashamba ya shule hiyo.

Sunday, April 24, 2011

PASAKA NJEMA


Bw.Benjamin J.Kaminyoge,anawatakia wakristo wote ulimwenguni heri ya sikukuu ya Pasaka,kwa kutumia sikukuu hii tusameane makosa yetu na kuwa na upendo.

MITAMBO YA KUPIMIA MITA ZA MAJI


Mdau wetu akiwa ametembelea mitambo maalumu inayotumika kupima mita za maji zenye matatizo huko Mbeya.

Sunday, April 17, 2011

MANCHESTER YAKABWA KOO


Manchester united jana imefungwa bao 1-0 na mahasimu wao Manchester City,katika michuano ya FA CUP,michuano hiyo imekuwa na msisimko mkubwa kwa timu ndogo kuzitoa jasho timu kubwa.

Saturday, April 16, 2011

AJALI MBAYA YATOKEA ARUSHA

Poleni ndugu zetu wa Arusha kwa msiba uliowapata  kutokana na ajali ya iliyohusisha basi la kampuni ya ngorika na basi dogo aina ya hiace na kusababisha vifo vya watu na wengine kujeruhiwa.

Thursday, April 14, 2011

SHITAMBALA AISALITI CHADEMA

Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha maendeleo mkoa wa Mbeya ameamua kuhama chama chake na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM,uamuzi wake umepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi mkoani Mbeya

Monday, April 11, 2011

YANGA BINGWA


Timu ya Yanga imetwaa ubingwa wa Tanzania bara baada ya kuifunga Toto African kwa jumla ya mabao 3-0,magoli ya Yanga yalifungwa na Nurdin Bakar na Davies Mwape yote kipindi cha pili,hivyo kuifanya Yanga kufikisha pointi 49 sawa na mahasimu wao Simba lakini wanakuwa mabingwa kwa tofauti ya magoli,Simba waliifunga Majimaji ya Songea bao 4-1.

Saturday, April 09, 2011

STENDI KUU MBEYA


Ukarabati unaoendelea ndani ya kituo cha mabasi Mbeya umesababisha lango la kutokea kufungwa kwa muda na kusababisha gari zote kuingia na kutokea mlango mmoja,imekuwa ni taabu hasa asubuhi zinapoondoka gari za mikoani.

Wanafunzi wakipata elimu kwenye ukumbi wa mikutano chini ya bwana Morgan Seben.

Wanafunzi wa Swaya sekondari wakipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa kitengo cha damu Mbeya bwana Morgan Seben walipotembelea kitengo hicho.


ZIARA YA WANAFUNZI WA SEKONDARI YA SWAYA-MBEYA.


Wanafunzi wa Swaya walipotembelea benki ya damu kwa ajili ya mafunzo juu ya mfumo wa damu.

Eneo la Kabwe Mbeya.

MVUA NDANI YA MBEYA


Baadhi ya mitaa jijini Mbeya imekuwa ni kero kutokana na mvua inayoendelea kunyesha na kusababisha barabara kujaa maji kutokana na mashimo kama inavyoonekana moja ya barabara eneo la Soweto.

YANGA YAKARIBIA UBINGWA


Timu ya Yanga imeamusha matumaini ya kutwaa ubingwa msimu huu baada ya kuwachapa African Lyon kwa jumla ya bao 3-0 na kufikisha pointi 46 na kubakiwa na mechi moja sawa na mahasimu wao Simba ambayo nayo imebakiza mchezo mmoja dhidi ya Majimaji.

Wednesday, April 06, 2011

SIMBA ALMANUSRA KWA RUVU JKT


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara Simba leo wamenusurika kichapo kutoka kwa maafande wa JKT RUVU baada ya kusawazisha bao kwa njia ya penati iliyofungwa na Emanuel Okwi,ilikuwa ni JKT RUVU iliyokuwa ya kwanza kujipatia bao la kuongoza kipindi cha kwanza lililowekwa kimiani na Hussein Bunu na kudumu hadi mapumziko,Simba ambao leo walionekana kubanwa vilivyo na wapinzani wao,mwamuzi wa mchezo huo alishindwa kuumudu mchezo huo na kuwatoa nje wachezaji wa JKT akiwemo Shabaan Dihile na George Minja,ligi hiyo itaendelea tena kesho kati ya Yanga dhidi ya African Lyon,Yanga wanahitaji ushindi ili kujiwekea mazingira mazuri ya kunyakua ubingwa.

VODACOM WABADILISHA RANGI YAO.


Linaloonekana ni jengo la Vodashop Mbeya,likiwa linaendelea kupigwa rangi tofauti na ile iliyozoeleka na wengi ya bluu sijui na jina litakuwaje?umekuwepo mchezo wa kubadili majina na rangi kwa baadhi ya makampuni ya simu kama vile mobitel wakaitwa Buzy na sasa tigo na Celtel wakaitwa Zain na sasa Airtel.

Friday, March 11, 2011

EARTH QUACKE JAPAN

Japan yatikiswa na tetemeko na kimbunga na kuharibu mali kadhaa ikiwemo majengo na miundo mbinu mbali mbali.

YUKO WAPI HUYU ?

KUNA UWEZEKANO UNAMFAHAMU MTU HUYU,MI SIMFAHAMU KABISA.

DAVIES MWAPE

Davies Mwape ni moja kati ya wachezaji hatari katika ligi kuu ya msimu huu,ni mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa wa kufumania nyavu za adui na mbinu kuwatoka walinzi wa timu pinzani,viongozi wa Yanga mtunzeni mchezaji huyu msije mkamfanyia AMBANI

Thursday, March 10, 2011

LOLIONDO STOP

Mch.Ambilikile Mwasapile akiwawekea dawa baadhi ya watu waliofika kwa ajili ya kupatiwa huduma hiyo,lakini hata hivyo serikali imesimamisha huduma hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi na usalama wa dawa hiyo

SIMBA YAZIKALIA AZAM NA YANGA

Timu ya Simba ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Tanzania bara jana walifanikiwa kuongoza ligi kwa kuifunga Ruvu shooting ya Pwani kwa bao 1-0 dakika ya 87 likifungwa na mchezaji Ally Ahmed 'Shiboli' aliyeingia dakika ya 79 kuchukua nafasi ya Mbwana Samata aliyebanwa vilivyo na mabeki wa Ruvu,sasa Simba imefikisha pointi 41 baada kucheza michezo 18,ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 39 huku Azam ikiwa na pointi 37 

Tuesday, March 08, 2011

Mchungaji AMBILIKILE MWASAPILE (kulia) akihojiwa na waandishi wa habari waliofika nyumbani kwake,mchungaji huyo amekuwa akitoa dawa kikombe kimoja kwa kila mgonjwa

WATU WAFURIKA KWA MCHUNGAJI

Umati wa watu unaendelea kufurika kwa mchungaji mstaafu mzee Ambilikile Mwasapile wilayani Ngorongoro,watu wamekuwa wakitoka sehemu mbambali kwa ajili ya kufuata tiba ya magonjwa mbalimbali ambayo yamekuwa hayatibiki hospitalini

Monday, March 07, 2011

LIVERPOOL YAWACHINJA MANCHESTER UTD.

LIVERPOOL jana imeweza kuwashikisha adabu Manchester United baada ya kuwafunga mabao 3-1,magoli ya liverpool yaliwekwa kimiani na Dirk Kuyt.

SIMBA NA YANGA NGUVU SAWA

Timu  zenye upinzani wa jadi kwenye soka la bongo Simba na Yanga jana zilitoka sare ya kufungana bao 1-1

Friday, March 04, 2011

CRDB WAFUNGUA TAWI JIPYA MWANJELWA- MBEYA

Waziri wa maji,Profesa Mark Mwandosya (watatu kushoto) akikata utepe kufungua tawi jipya la benki ya CRDB eneo la Mwanjelwa jijini MBEYA,kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo bw.Martin Mmari,kulia ni mama Mwandosya,kufunguliwa kwa tawi hilo kutawasaidia wakazi wa jiji la Mbeya ambao walikuwa wakipanga foleni kwenye tawi pekee lililokuwa mjini Mbeya.

Wednesday, March 02, 2011

SOKO LA BIG BROTHER UBUNGO LAVUNJWA

Soko la big brother eneo la ubungo limevunjwa jana usiku ili ujenzi wa stend wa mabasi yaendayo kasi,hapa ni baadhi ya wafanyabiashara wakiangalia mabaki ya vibanda vyao.

GADAFFI ANG'ANG'ANIA MADARAKANI

  • Kiongozi wa Libya Muamar Gadaffi ameendelea kung'ang'ania madaraka,licha ya kuwepo kwa maandamano ya kumtaka kuachia madaraka hayo ya urais ambayo ameshikilia kwa zaidi ya miaka arobaini,amekuwa ahamini kinachotokea kwenye taifa lake kutokana na jinsi utawala wake kutowapa uhuru waandishi wa habari na redio.


WAZIRI MKUU AKIWA NA MABALOZI WA UFARANSA NA UINGEREZA

Waziri mkuu Mh.Mizengo Pinda ( kushoto) akiwa na balozi wa Ufaransa bwana Jacques Champagne De Labriolle na balozi wa Uingereza bibi Dianne Corner wakati wa mkutano wa wataalam wa uchumi leo jijini Dar es salaam.

Tuesday, March 01, 2011

Saturday, February 26, 2011


Wakazi wa Gongo la mboto wakishangaa bomu lililokita chini siku chache baada ya milipuko eneo hilo.

Thursday, February 17, 2011

MABOMU GONGO LA MBOTO


Madaktari wa hospitali ya Amana jijini Dar es salaam,wakimuhudumia mmoja wa waathirika wa mabomu hayo ambayo yalilipuka kutoka kwenye ghala la kutunzia silaha la JWTZ.

BREAKING NEWS!!!


Kuna mlipuko mkubwa unaendelea usiku huu eneo la Gongo la mboto jijini Dar es salaam,inasadikiwa ni kutoka kambi ya jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) na hivyo kuwafanya wakazi na majirani wa eneo hilo kuyakimbia makazi yao na kuelekea katikati ya jiji na kusababisha msongamano mkubwa kwenye baadhi ya barabara.
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kutoka mfuatiliaji wa taarifa hii.

Monday, February 14, 2011

SIMBA YAFUTA AIBU


Mabingwa wa soka Tanzania bara wamefanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kuifunga Elan club de mitsoudje ya Comoro kwa jumla ya magoli 4-2,Elan ndio iliyokuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 42 likifungwa na Madaha Mohamed,Simba walisawazisha dak 44 kupitia kwa Mbwana Samata,magoli mengine ya Simba yalifungwa na Patrick Ochan dk 47,Samata dk.56,Amri Kiemba dk.72 na goli la pili la Elan lilifungwa na Abdoulhouda Abdouleafor dk.63,nao mahasimu wao Yanga wameendelea kukumbwa na jinamizi la mechi za kimataifa baada ya kukubali kipigo cha 2-0 kutoka kwa Dedebit mchezo huo ulichezwa jana jijini Adis Ababa-Ethiopia,kwa matokeo hayo Simba itakutana na mabingwa watetezi TP Mazembe ya DRC.

Sunday, February 13, 2011

BOMOA BOMOA


Jengo jipya lililoko Mbeya eneo la Mafiat,likionekana limebomolewa upande kutokana na mmiliki wake kushindwa kuzingatia umbali kati ya barabara na nyumba.

Tuesday, February 08, 2011

Saturday, February 05, 2011

AZAM FC YAZIDI KUTISHA


Timu ya Azam imezidi kujiwekea mazingira mazuri ya kuwania ubingwa wa Tanzania bara baada kuwafunga Toto African mabao 3-0,mabao yao yalipachikwa dakika ya kwanza na 35 na John Boko(Adebayor) na bao la tatu lilifungwa dk ya 56 na Mrisho Ngasa baada ya kupata pasi kutoka kwa Ramadhan Chombo Ridondo,Toto African walipoteana baada ya kufungwa bao la mapema na hivyo kuwafanya Azam kumiliki mchezo huo na kufikisha 29 nyuma ya Yanga yenye pointi 31
na Simba yenye pointi 30 na hivyo kuongeza ushindani wa kuwania ubingwa,ligi hiyo itaendelea tena leo ambapo Yanga watakuwa wageni wa wanalizombe Majimaji huko Songea na AFC Arusha watawakaribisha JKT Ruvu pale Sheikh Amri Abeid mjini Arusha na kesho mabingwa watetezi Simba watashuka uwanja wa Jamhuri Dodoma kukabiliana na Polisi Dodoma.

Wednesday, February 02, 2011

YANGA YAPOKEA KICHAPO CHA KWANZA.


Timu ya Yanga leo imepoteza mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar ikiwa ni mchezo wake wa kwanza kupoteza toka ligi kuu ya msimu kuanza,kutokana na Yanga kucheza chini ya kiwango ilimulazimu kocha wake Fred Felix Minziro Kataraia(baba Isaya au Majeshi) kusimama muda wote na kuliona benchi chungu baada ya Mtibwa kutawala mchezo huo,mara baada ya mchezo huo kumalizika mashabiki wanaosadikiwa kuwa ni wa Yanga waliwafanyia vurugu wachezaji wa Yanga kwa kutoridishwa na mwenendo wa timu hiyo na kutokuwepo kwa wachezaji kama Shadrack Nsajigwa,Yaw Berko,Athman Idd kunaonekana kuwaathiri Yanga kwenye mechi ya leo bila kumsahau kocha Costadin Papic ambaye ametimkia Africa Kusini kutokana na kutokuelewana na baadhi ya viongozi wa timu hiyo ambayo pia inakabiliwa na mechi ya kombe la shirikisho Africa dhidi Dedebit ya Ethiopia kwenye mchezo wa marudiano.