BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Thursday, December 01, 2011

TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA


leo ni siku ya maadhimisho ya ukimwi duniani,ugonjwa ambao umekuwa ukiwasumbua watu wengi duniani inakadiriwa kuwa kuna watu zaidi milioni 34 wanaishi na maambukizi ya ugonjwa huo,inonekana nchi za kusini mwa jangwa la sahara ndizo zenye wagonjwa wengi,imekuwa zikifanyika jitihada mbali mbali kuhakikisha maambukizi ya ugonjwa huu yanapungua au kuutokomeza kabisa kwa kuwaelimisha watu.

Friday, November 25, 2011

MAFURIKO YALETA MAAFA MONDULI

 Baadhi ya picha zinnazoonyesha maafa yaliyotokana na mafuriko huko Monduli na miundo mbinu kuharibika





 Mwili wa marehemu ukiwa umenaswa kwenye vichaka

 Magari nayo yalibebwa na mafuriko hayo

MVUA YANYESHA KWA MUDA MREFU MBEYA.


Jiji la Mbeya leo limekuwa na neema baada ya mvua kunyesha kwa takribani masaa 10,na kusababisha watu kushindwa kuwahi makazini.

Wednesday, November 23, 2011

CHANGIA DAMU OKOA MAISHA


Damu ni tiba inayotokana na binadamu wenyewe kwa maana hiyo sisi ndio wenye jukumu la kuchangia damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu wanaohitaji tiba hiyo na kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji tiba hiyo,kwa wale wale walioko Mbeya unaweza ukafika kwenye kituo cha damu salama kilichoko hospitali ya wazazi Meta,Mwanza damu salama Bugando,kwa wale walioko Dar es salaam na maeneo jirani mtafika kituo cha damu salama kilichoko Mchikichini,Moshi mkabala na hospitali KCMC,Mtwara kituo cha damu salama Mtwara na Tabora fika kwenye kituo cha damu salama Tabora-CHANGIA DAMU MARA KWA MARA ILI UOKOE MAISHA.

PAPA BENEDICT XVI KUTEMBELEA BENIN


Kiongozi wa kanisa la katoliki duniani,Papa Benedict wa 16 anatarajia kutembelea nchi ya Benin wiki hii.
Hii ni ziara ya pili kwa Papa Benedict barani Africa tangu kuteuliwa kwake,na ni mara ya tatu kwa taifa la Benin kutembelewa na uongozi wa juu wa kanisa hilo,mwaka 1982 na 1993 walitembelewa na Papa John Paul II.
Msemaji wa Vatican amesema ziara hiyo ni ya kuleta amani na maridhiano barani Afrika.

AJALI MBAYA YATOKEA UBUNGO RIVER SIDE


 Wananchi wakijaribu kuokoa maisha ya watu waliokuwa kwenye gari dogo lililoingia uvunguni mwa lori eneo la Ubungo river side mchana wa leo
Wananchi wakiangalia ajali ambayo imepoteza maisha ya watu watatu na mmoja akiwa hai ndani ya gari dogo,jitihada za kumtoa zinaendelea kufanyika


TUKUYU NI NEEMA TU

Wakina mama wa eneo la Kiwira wakiuza matunda ya aina mbalimbali kwa wageni na wenyeji wa wanaopita kwenye barabara ya Dar-Malawi.


Wakina mama wakisubiri wateja wa ndizi eneo la Kiwira

Eneo hili ndilo linlofanyiwa biashara eneo la Kiwira,licha kukaa kihatarihatari


Wakina mama wakiuza ndizi,maparachichi,mananasi nk.kwenye basi linalofanya safari kati ya Mbeya na Kyela


MACHAFUKO MENGINE CAIRO

Hali inaelekea kuwa mbaya zaidi mjini Cairo kutokana na jeshi kutumia nguvu zaidi kwa ajili ya kuwadhibiti waandamanaji wanaoshinikiza utawala wa kijeshi kuondoka madarakani,tayari mpaka sasa zaidi watu 30 wanahofiwa kupoteza maisha kwenye machafuko yanayoendelea jijini Cairo,na sasa machafuko hayo yamemeanza kwenye miji ya Alexandria,Suez,Port Said na Aswan


Mmoja wa majeruhi akipata huduma ya kwanza

Hili ni eneo la Tahrir jijini Cairo ambalo linaonekana kuwa na vurugu zaidi

Thursday, November 17, 2011

UHABA WA MAJI WATISHIA USALAMA WA AFYA ZA WANANCHI MBALIZI.


Kufuatia uhaba wa maji uliyoukumba mji mdogo wa Mbalizi na vitongoji vyake,na kusababisha wakazi wa maeneo hayo kuchota maji na kufulia kwenye kwenye mifereji na mito,kunaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa kutokana na mji huo kuwa na wakazi wengi na biashara nyingi.

Tuesday, November 15, 2011

LORI LANUSURIKA NA KUZIBA BARABARA.


Lori la mizigo aina ya Scania,jioni hii limenusurika kuanguka baada ya kuacha njia na kuingia kwenye mtaro ulioko kando ya barabara na kurudi tena barabarani na kuziba barabara kwa muda na kusababisha magari makubwa kushindwa kupita,ajali imetokea leo jioni eneo la Ntokela,barabara ya Uyole-Tukuyu,hakuna mtu aliyejeruhiwa kwenye ajali hiyo.

Sunday, November 13, 2011

MAREKANI YAOMBA MSAMAHA KWA INDIA


Marekani imeiomba msamaha serikali ya India kutokana na kitendo cha maafisa wake wa uwanja wa ndege wa New York kumpekua rais wa zamani wa India,bwana Abdul Kalam mwezi Septemba.
Serikali ilitoa malalamiko yake kwa Marekani kufuatia kitendo hicho kilichoonekana kama udhalilishaji kwa mheshimiwa huyo,pia mcheza sinema maarufu wa India Shah Rukh Khan aliwahi kulalamikia kitendo kama hicho alichofanyiwa mwaka 2009.

Friday, November 11, 2011

Taifa Stars yaichapa Chad 2-1


Timu ya soka ya Tanzania leo imefanikiwa kupata ushindi ugenini kwa kuichapa timu ya taifa ya Chad mabao 2-1,mabao ya Taifa Stars yamefungwa na Mrisho Ngasa na Nurdin Bakar.

VURUGU ZATAWALA MBEYA LEO


Askari wa jeshi la polisi wakijaribu kutuliza ghasia maeneo ya tukio jijini Mbeya

Gari likiwa limebinuliwa na waandamanaji na kufunga barabara kuu ya Dar-Tunduma eneo la Kabwe


Matairi chakavu yakiwa yamechomwa katikati ya barabara  na kuleta taabu kwa wasafiri na moshi mzito kusambaa eneo la Kabwe (Picha kwa hisani ya  Mwaisango)


Thursday, November 10, 2011

WAKULIMA WA MANANASI RUNGWE WANAHITAJI SOKO LA UHAKIKA ILI KUBORESHA KILIMO CHA MATUNDA HAYO



Mfanyabiashara wa mananasi akikusanya mananasi kutoka kwa wakulima wa Ikuti wilayani Rungwe 


Wakazi wa kijiji cha Ikuti hujipumzisha maeneo haya mara baada ya kumaliza shughuli zao za kila siku
 

Wednesday, November 09, 2011

BONDIA JOE FRAZIER AFARIKI DUNIA


Aliyekuwa nguli wa mchezo wa masumbwi kwenye miaka ya 60 na 70,Frazier amefariki juzi baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa saratani ya ini.
Frazier alikuwa bondia wa kwanza kumpiga bingwa wa kipindi hicho Muhammad Ally katika mpambano uliochezwa DR Congo machi, 1971,amefariki akiwa na umri wa miaka 67,wapenzi wa mchezo huo wataendelea kumkumbuka kutokana na umahiri wake ulingoni na hasa kwa kumchapa bingwa aliyeshindikana Muhammad Ally.

Monday, November 07, 2011

WATOTO WANAPENDA KUPENDWA


Watoto wa shule ya msingi Itenya,kijiji cha Ngonga wilayani Kyela wakiwa na bw Benjamin alipopita maeneo ya kijiji hicho

Thursday, November 03, 2011

IRINGA YAENDELEA KUKUA KWA KASI


Mdau wetu akiwa kwenye kijiji cha Ilambilole wilayani Kilolo

Hapa akiwa mtaa wa Mshindo Iringa mjini

Mdau wetu akiwa kituo cha mabasi ya kwenda mikoani mjini Iringa

Kati ya vivutio vilivyoko mkoani Iringa ni pamoja na mawe mazuri yaliyo kando ya barabara kuu

Tuesday, November 01, 2011

MASELE NA WENZAKE WAWALEMAZA WASAFIRI KITUO CHA MABASI MBEYA.


Msanii maarufu na wenzake toka jijini Dar es salaam,leo wamewateka wasafiri waliokuwepo kituo kikuu cha mabasi jijini Mbeya,na kuwafanya wabaki wakiwaangalia na kusahau kufanya mipango ya safari kutokana na vituko vyao vya maigizo walivyokuwa wakionyesha na kuwavutia wasafiri wengi na baadhi wafanyabiashara wa eneo hilo.

Saturday, October 29, 2011

YANGA YAICHAPA SIMBA 1-0


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara leo wameichapa Simba bao 1-0 kwenye mchezo wa ligi kuu uliyofanyika uwanja wa Taifa,Yanga walipata bao hilo dakika ya 72 kupitia kwa mshambuliaji wao wa kimataifa Davies Mwape baada ya walinzi wa Simba kufanya makosa,mchezo huo ulianza kwa kasi na Simba kutawala kipindi cha kwanza,Simba walipoteza nafasi kadhaa kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili Yanga walijipanga na kubadili mchezo na hivyo kuwafanya waibuke na ushindi huo.
Michezo mingine ya ligi hiyo imechezwa huko Mwanza kati ya Toto African na Coastal Union matokeo ni 0-0,huko Dodoma ilikuwa ni kati ya Polisi na Oljoro matokeo ni 0-0,kwa matokeo haya bado hayabadili msimamo wa ligi bado Simba inaongoza ligi ikiwa na alama 27,ikifuatiwa na Yanga yenye alama 24,Azam 21.

Monday, October 24, 2011

MANCHESTER CITY YAWAFANYIA VIBAYA MANCHESTER UNITED NDANI YA OLD TRAFFORD


Timu ya Manchester City leo imevunja mwiko wa Manchester United baada ya kuwaadhibu kwa goli 6-1 kwenye uwanja Old Trafford.
Manchester Utd imekuwa na rekodi ya kutofungwa kwenye uwanja wa nyumbani lakini leo imeweza kutokea tena idadi kubwa ya magoli.

Thursday, October 20, 2011

GADAFFI AFA KISHUJAA

Aliyekuwa rais wa Libya Muamar Gadaffi leo ameuawa na jeshi la waasi lililom
muondoa madarakani baada ya kumshika na kumjeruhi kwenye mji wake alikozaliwa na kupelekea kifo chake.
 Gadaffi tofauti na marais wengine yeye aliendelea kubakia nchini kwake pamoja na sehemu ya nchi kushikiliwa na waasi,aliendelea na kuishi kwenye mji wa Sirte ambako ndiko alikozaliwa.

Tuesday, October 18, 2011

HUU NDIO USAFIRI WA MLOWO-KAMSAMBA WILAYANI MBOZI.


Pamoja na ajali nyingi kugharimu maisha ya watu,lakini bado watu wamekuwa wakijisahau na kuvunja sheria za usalama barabarani kama inavyoonekana hapa gari ya mizigo ikiwa imebeba abiria wengi kupita kiasi na wengine kukaa juu ya mabomba.

Sunday, October 16, 2011

LIVERPOOL YAWATOA ULIMI NJE MANCHESTER UNITED


Timu ya Liverpool ikicheza kwa maelewano jana iliweza kutoka sare na Manchester Utd kwa kufungana bao 1-1 kwenye uwanja Anfield,Liverpool walipata bao dakika ya 67 kupitia kwa Steven Gerrald na Manchester walisawazisha dak.80 kupitia kwa Chicharito.
Liverpool walitawala mchezo huo kwa kiasi kikubwa na kuwafanya walinzi wa Man kuwa na wakati mgumu.

Saturday, October 15, 2011

LIGI DARAJA LA KWANZA,PRISON YAANZA VIBAYA MBEYA


Timu ya Tanzania Prison leo imeanza vibaya baada ya kufungwa bao 1-0 na timu ya Mbeya City Council,bao la Mbeya City limefungwa na Yona Ndabila kwa njia ya penati kipindi cha kwanza,hadi mapumziko Prison walikuwa nyuma kwa bao 1

Tuesday, October 11, 2011

TUWE NA MOYO WA KUJITOLEA DAMU KWA AJILI YA KUWASAIDIA WAGONJWA MAHOSPITALINI

Darling Lyatuu naye akichangia damu siku ya leo chini ya uangalizi wa mtaalamu wa kitengo cha taifa cha damu salama bi.Joyce Yonael Msuya.