BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, June 28, 2011

GODWIN FRANCIS AKIWA KAZINI GANGILONGA


Mmiliki wa mtandao wa godwinfrancis.blogspot.com akiwa juu ya jiwe la Gangilonga,katika ziara yake ya kutembelea vivutio mkoani Iringa ambavyo havijaorodheshwa mkoani Iringa.

BEI YA MAFUTA YAATHIRI WENGI


Picha inayoonekana ni mwili wa marehemu ukifungwa kwenye pikipiki tayari kwa safari ya kuelekea kijiji cha Isansa wilayani Mbozi kutoka wilaya Mbeya,inaonekana ni kitu cha ajabu lakini ndio halisi iliyotokea,inakadiriwa kuwa kufika kijijini kwao ni zaidi kilomita 90 kama wangetumia gari ingewagharimu kuliko uwezo wao,hii inaashiria wananchi wanavyoishi kwa taabu na kubuni njia mbadala za kutatua matatizo yao bila kujali athari zinazoweza kutokea.

DALADALA BALAA


Jioni hii daladala iliyokuwa ikitokea eneo la Soko Matola kuelekea Iyunga,imegonga gari ndogo aina ya Toyota Corolla eneo la Sabato ndani ya gari hiyo alikuwemo mdau wa blog hii,hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa kwenye ajali hii.

Gari ndogo ambayo imegongwa na daladala

WAFANYABIASHARA SOKO LA UHINDINI MBEYA WAHAMIA ENEO JIPYA

Hili ni eneo la uwanja wa Sokoine Mbeya ambalo wafanyabiashara wa soko la uhindini wamehamia baada ya soko lao walilozoea kuungua moto mapema mwaka huu.
 Baadhi ya mafundi wakimalizia vyumba eneo la uwanja wa Sokoine Mbeya
 
Wauzaji matunda na mbogamboga kwenye soko hilo

Monday, June 27, 2011

PRESIDENT Dr.J.KIKWETE SIGNS A CONDOLENCE BOOK AT ZAMBIAN HIGH COMMISSION IN DAR ES SALAAM TO MOURN CHILUBA

President Dr.Jakaya M.Kikwete signs a condolence  book at the Zambian high commissioner's residence in  Dar es salaam this morning,following the death of former  Zambian President  Fredrick Chiluba early last week.

Sunday, June 26, 2011

YANGA ULIMI NJE KWA EL-MEREIKH


Leo El-mereikh imewalazimisha mabingwa wa Tanzania bara timu ya Yanga sare ya bao 2-2 kwenye mchezo uliofanyika uwanja wa Taifa,El-mereikh waliweza kuwatawala Yanga kipindi cha pili kwa kucheza jinsi wanavyotaka na kufanikiwa kusawazisha bao la pili,Yanga kipindi waliingia cha pili safu ya kiungo ilikuwa imezidiwa na kuwapa nafasi El-mereikh kutawala mpira.

KAGAME CUP YAANZA


Michuano ya kuwania ubingwa wa Afrika mashariki na kati imeanza kwa mechi za ufunguzi,zimepigwa mechi mbili,katika mechi ya kwanza timu ya Ocean view imeilaza timu ya Eticele ya Ruanda 3-2,huku Simba ikitoka 0-0 na vitalo ya Burundi,mechi hizo zitaendelea tena kwenye viwanja vya Jamhuri Morogoro na uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Friday, June 24, 2011

CHUO KIKUU CHA UFUNDI MBEYA (MIST)


Hili ni eneo la ofisi za utawala za chuo kikuu cha ufundi Mbeya,ambacho zamani kilijulikana kama Mbeya Technical College,leo ni chuo kikuu ambacho tunategemea kitatoa waandisi wa kada mbalimbali na kuliepusha taifa kuwa tegemezi kwenye upande wa wataalamu kutoka nje

Haya ni baadhi ya majengo ya chuo kikuu cha ufundi (MIST) Mbeya.

Thursday, June 23, 2011

MICHELLE OBAMA AKUTANA NA NELSON MANDELA


Mke wa rais Barack Obama,bi.Michelle Obama amekutana na mzee Mandela na kufanya mazungumzo naye,Michelle yuko ziarani Afrika kusini.

Wednesday, June 22, 2011

HIKI NDIO KIKOSI CHA YANGA KILICHOTWAA UBINGWA WA AFRIKA MASHARIKI NA KATI MWAKA 1998



MORAVIAN KUWEKA MAKAO MAKUU DODOMA


Askofu Alenikisa Cheyo amesema kanisa la Moravian liko mbioni kuhamishia makao makuu mjini Dodoma,alikuwa akizungumza kwenye harambee iliyofanyika kanisa la Ruanda Mbeya

BAJAJ YAJERUHI ABIRIA


Mwanamke mmoja amejeruhiwa baada ya pikipiki ya tairi au Bajaj kugonga gari ndogo aina ya Carina eneo la mikocheni jijini Dar es salaam

Tuesday, June 21, 2011

UTUNZAJI WA KUMBU KUMBU NI MUHIMU

Baadhi ya wananchi waliotembelea banda la idara ya habari maelezo wakiangalia photo album za matukio ya uhuru wa Tanganyika,huku tukijiandaa na maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru-Mungu ibariki Tanzania.

DAWA FEKI YA KUKUZA MAKALIO HII HAPA

Ofisa uhusiano wa mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) Bi.G.Simwanza akionesha dawa feki ya kuongeza ukubwa wa makalio katika banda la TFDA kwenye maadhimisho ya utumishi wa umma ya umoja wa mataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya mnazi mmoja

Monday, June 20, 2011

KANISA LA MORAVIAN KUHAMISHIA MAKAO MAKUU MJINI DODOMA

                                                                  Kanisa la Moravian liko kwenye mipango ya kuhamishia makao makuu ya kanisa hilo mjini Dodoma hayo yameelezwa na Askofu mkuu wa kanisa ndg.Alinikisa Cheyo katika ibada ilyofanyika jana kwenye kanisa la Ruanda Mbeya,alisema tayari wameshapata ekari 225 kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya ofisi na vitega uchumi mbalimbali pia alielezea kuwa wako kwenye mipango ya kufungua campus ya chuo kikuu kinachomilikiwa na kanisa hilo kwenye mikoa ya Tabora na Dar es salaam na wanategemea kuanza september mwaka huu.

UJENZI WA KITUO CHA DALADALA CHA MBEZI SASA WAELEKEA KUKAMILIKA

Kituo kipya cha daladala cha Mbezi sasa kipo katika hatua za mwisho mwisho kama picha hii inavyoonyesha

Saturday, June 18, 2011

CYNTHIA KIMASHA AWA MISS VODACOM CHANG'OMBE

Cynthia Kimasha (katikati) amefanikiwa kutwaa taji la vodacom miss Chang'ombe,huku mshindi wa pili akiwa Husna Twallib (kushoto) na mshindi wa tatu ni Joyce Maweda,shindano hilo limefanyika kwenye viwanja vya Tcc Chang'ombe.
Hawa ndio walifanikiwa kuingia tano bora kwenye shindano hilo

CHILUBA AFARIKI DUNIA

Aliyekuwa rais wa pili wa Zambia bw.Fredrick Titus Chiluba amefariki usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake,Chiluba ameiongoza Zambia toka 1991-2002 na hadi kifo chake akikuwa na tuhuma ya ubadhirifu wakati wa uongozi wake

Friday, June 17, 2011

AIRTEL DONATES BLOOD TO SUPPORT CHILDREN WITH CANCER

Mr.D.Kaimukiwa ,a physician from the National blood transfusion service(left) collecting blood from Mohamed Gulamali,Airtel staff in Dar es salaam.Airtel Tanzania orgarnized a one day blood donation drive to support the children with cancer.

BAMBO APATA AJALI YA PIKIPIKI

Msanii maarufu katika ya fani ya uigizaji nchini bw.Dickson Samson Makwaya a.k.a BAMBO amepata ajali ya pikipiki eneo njia panda kigogo jijini Dar es salaam,na kuvunjika mguu wa kulia amelazwa hospitali ya taifa Muhimbili

Tuesday, June 14, 2011

SIKU YA WACHANGIA DAMU DUNIANI

Bi.Tumaini Kanyamale akiwa na mtaalamu kitengo cha damu Mbeya bi.Salome magwaza.
Leo ni siku ya wachangia damu kwa hiari duniani,maadhimisho haya hufanyika kila june 14,picha inayoonekana ni bw.Paul Haule mkazi wa Nzovwe Mbeya akichangia damu katika siku hii kwenye kitengo cha damu salama akiwa na mtaalamu wa kitengo hicho bi. Salome Magwaza.Kumbuka damu haiuzwi

Sunday, June 05, 2011

TAIFA STARS YACHAPWA TENA,U-23 YAIFUNGA NIGERIA 1-0


Timu ya Taifa ya Tanzania leo imefungwa na timu ya taifa ya Africa ya kati bao 2-1 kwenye uliofanyika uwanja wa Complex Barthelemy Bonganda mjini Bangui huko Africa ya kati,kwenye mchezo mwingine timu ya vijana ya chini ya miaka 23 leo imefanikiwa kuwafunga wenzao wa Nigeria bao 1-0,Tanzania walipata bao dakika ya 84 likiwekwa kimiani na Thomas Ulimwengu kwenye uwanja Taifa jijini Dar es salaam

Thursday, June 02, 2011

AJALI NYINGINE MBEYA


Basi la kampuni ya Abood jana lilianguka eneo la mlima nyoka na kujeruhi abiria 36,kwa bahati nzuri halikusababisha vifo kwa abiria wake,huu ni mfululizo wa ajali kutokea mkoani Mbeya,Ijumaa iliyopita basi la Sumry lilipata ajali na kupoteza maisha ya watu 13 na wengine kadhaa kujeruhiwa,Abood ilikuwa ikitokea Dar es salaam kuja Mbeya.

MAFUNZO YA UZIMAJI MOTO


Bw.Hashim Yahya Mbelwa akitoa elimu kwa wafanyakazi wa BTS jinsi ya kuzima na kukabiliana na moto kwenye ukumbi wa BTS semina hiyo ilikuwa nzuri na kueleweka na kila mmoja.

MAFUNZO YA UZIMAJI MOTO


Bw.Hashim Yahya Mbelwa akitoa elimu kwa wafanyakazi wa BTS jinsi ya kuzima na kukabiliana na moto kwenye ukumbi wa BTS semina hiyo ilikuwa nzuri na kueleweka na kila mmoja.

MAFUNZO YA KUZIMA MOTO


Bi Helen Kataraiya akifanya moja ya majaribio ya kuzima moto huku akisimamiwa na mmoja wa wakufunzi wa semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa BTS Mbeya,moto ni rafiki haumchokozi mtu mpaka ukosewe.

Tuesday, May 31, 2011

MSIBA


Mwili wa marehemu magreth Komba ukipakiwa kwenye gari tayari kwa mazishi yatakayofanyika eneo la Uyole Mbeya kabla ya kufanyiwa swala na viongozi wa dini.

Wauguzi na madaktari wa hospitali ya rufaa Mbeya, wakitoa heshima za mwisho kwa mtumishi mwenzao Magreth Komba pamoja na mumewe waliofariki kwa ajali ya basi.

Monday, May 30, 2011

MBEYA (MAPINDUZI STARS) WAPOKELEWA KWA VIFIJO NA NDEREMO.


Golikipa wa mkoa wa Mbeya Ivo Mapunda akimkabidhi kombe la ubingwa wa taifa mkuu wa mkoa wa Mbeya mh.John Mwakipesile leo katika hafla fupi ya kuwapokea mashujaa hao wa mkoa wa Mbeya mara baada ya kurejea kutoka Arusha-picha kwa hisani ya mbeya yetu blogspot.com

Mchezaji bora wa kombe la Taifa kwa mwaka 2011 Juma Mpola akiwa na daktari wa timu ya mkoa wa Mbeya wakiwa kwenye trela la TBL ambao ni wadhamini wa Kombe la Taifa kwa kupitia bia yao ya kilimanjaro

Sunday, May 29, 2011

BARCELONA BINGWA ULAYA


Timu ya Barcelona imetwaa ubingwa wa ulaya baada kuwachapa Manchester united bao 3-1,goli la kwanza la Barca liliwekwa kimiani na Pedro na Man walisawazisha kupitia Wayne Rooney hadi mapumziko timu hizo zilikuwa nguvu sawa,kipindi cha pili Barcelona walifanikiwa kupata mabao mawili kupitia kwa Leone Messi na David Villa mechi hiyo imechezwa kwenye uwanja wa Wembley jijini London.

Saturday, May 28, 2011

WYDAD CANSABLANCA YAICHAPA SIMBA 3-0.


Timu ya Simba leo imefungwa jumla ya mabao 3-0 na Wydad Cansablanca ya Morroco magoli ya wamorroco hao yamefungwa dakika ya 87 na mengine mawili yakifungwa dakika za majeruhi,mchezo huo umechezwa kwenye uwanja Petrosport jijini Cairo,na hivyo kuzima ndoto za Simba kucheza hatua ya makundi klabu bingwa Africa,sasa wataingia kwenye michuano ya kombe la shirikisho na kucheza na Motema Pembe ya Congo

MBEYA BINGWA KOMBE LA TAIFA


Timu ya mkoa wa Mbeya leo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe la taifa baada ya kuifunga timu ya mkoa wa Mwanza kwa bao 1-0,bao pekee la Mbeya limefungwa dakika ya 87 na mshambuliaji tishio nchini Gaudence Mwaikimba.

BASI LA TAQWA LAANGUKA.


Zaidi ya abiria 50 wamenusirika kifo baada ya basi la taqwa kuanguka eneo la Iyofi mpakani mwa mikoa ya Morogoro na Iringa,basi hilo lilikuwa likielekea jijini Dar es salaam.

SUMRY YAPATA AJALI MBAYA.


Basi la kampuni ya Sumry high class limepata ajali eneo la Igawa na kupoteza maisha ya abiria 13 na wengine kujeruhiwa,basi hilo lilipata ajali kutokana na kupasuka tairi la mbele na kusababisha basi hilo kupinduka,basi hilo lilikuwa likitokea jijini Arusha.

Wednesday, May 25, 2011

OBAMA ASEMA LAZIMA GADAFFI AONDOKE


Rais Barack Obama amesema lazima rais Muamar Gadaffi aondoke madarakani,ameyasema katika yake nchini Uingereza,nchi imekuwa na machafuko ya kisiasa kwa mitatu na zaidi,huku nchi za ulaya zikionekana kuwaunga mkono waasi wa serikali ya Libya.

MBEYA YAINGIA FAINALI KOMBE LA TAIFA


Timu ya mkoa wa Mbeya(Mapinduzi stars) imefanikiwa kuingia fainali ya michuano ya kombe la taifa,baada ya kuifunga timu ya mkoa wa Kagera kwa jumla ya mabao 2-1,mchezo huo umechezwa kwa dakika 120,hadi dakika 90 zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana 1-1,Mbeya ndio waliofanikiwa kupata ushindi baada ya beki wa Kagera kujifunga baada ya shambulizi kutokea golini kwao,mchezo huo ulikuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote kucheza soka maridadi na golikipa wa Mbeya Ivo Mapunda kuonyesha uwezo mkubwa,Mbeya watakutana na Mwanza Heroes siku ya jumamosi uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha katika fainali.

Thursday, May 19, 2011

SIMBA KUVAANA NA WYDAD CANSABLANCA CAIRO

Timu ya Simba imfanikiwa kurudi kwenye michuano ya klabu bingwa Africa baada ya rufaa yao kukubaliwa na shirikisho la soka Africa(CAF) na kuitupia mbali timu ya TP Mazembe ambao ndio mabingwa wa kombe hilo baada ya kumchezesha mlinzi halali wa timu ya Esperence ya Tunisia,sasa simba watacheza na wydad cansablanca ya Morocco kwenye uwanja huru huko jijini Cairo

AJALI MBAYA GEITA

Ajali mbaya imetokea Geita baada ya basi la sheraton kugongana na lori na kusababisha watu kumi na sita kupoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa

Sunday, May 15, 2011

AJALI


Gari kubwa aina ya scania likiwa limeacha njia na kujikita kwenye mitaro iliyopo pembeni ya barabara,eneo la Iwambi Mbeya.

Msongamano huu umesababishwa na lori liliacha njia na kujikita kwenye mtaro wa barabara eneo la Iwambi-Mbeya.

Thursday, May 12, 2011

MAMA NA MWANA

Mama Mchungaji wa kanisa la moravian usharika wa NZOVWE  mama Salome Kalengo,akiwa na watoto wake walipotembelea ofisini kwake

Sunday, May 08, 2011

MANCHESTER UTD YAICHAPA CHELSEA 2-0


Manchester utd imezidi kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa England baada ya kuwachapa Chelsea kwa bao 2-0,na hivyo kuwa mbele kwa pointi 6 na zikiwa zimebakiwa na mechi 2 nao Arsenal wamepokea kichapo cha bao 3-1 kutoka kwa Stoke City.