BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, June 18, 2011

CHILUBA AFARIKI DUNIA

Aliyekuwa rais wa pili wa Zambia bw.Fredrick Titus Chiluba amefariki usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake,Chiluba ameiongoza Zambia toka 1991-2002 na hadi kifo chake akikuwa na tuhuma ya ubadhirifu wakati wa uongozi wake

Friday, June 17, 2011

AIRTEL DONATES BLOOD TO SUPPORT CHILDREN WITH CANCER

Mr.D.Kaimukiwa ,a physician from the National blood transfusion service(left) collecting blood from Mohamed Gulamali,Airtel staff in Dar es salaam.Airtel Tanzania orgarnized a one day blood donation drive to support the children with cancer.

BAMBO APATA AJALI YA PIKIPIKI

Msanii maarufu katika ya fani ya uigizaji nchini bw.Dickson Samson Makwaya a.k.a BAMBO amepata ajali ya pikipiki eneo njia panda kigogo jijini Dar es salaam,na kuvunjika mguu wa kulia amelazwa hospitali ya taifa Muhimbili

Tuesday, June 14, 2011

SIKU YA WACHANGIA DAMU DUNIANI

Bi.Tumaini Kanyamale akiwa na mtaalamu kitengo cha damu Mbeya bi.Salome magwaza.
Leo ni siku ya wachangia damu kwa hiari duniani,maadhimisho haya hufanyika kila june 14,picha inayoonekana ni bw.Paul Haule mkazi wa Nzovwe Mbeya akichangia damu katika siku hii kwenye kitengo cha damu salama akiwa na mtaalamu wa kitengo hicho bi. Salome Magwaza.Kumbuka damu haiuzwi

Sunday, June 05, 2011

TAIFA STARS YACHAPWA TENA,U-23 YAIFUNGA NIGERIA 1-0


Timu ya Taifa ya Tanzania leo imefungwa na timu ya taifa ya Africa ya kati bao 2-1 kwenye uliofanyika uwanja wa Complex Barthelemy Bonganda mjini Bangui huko Africa ya kati,kwenye mchezo mwingine timu ya vijana ya chini ya miaka 23 leo imefanikiwa kuwafunga wenzao wa Nigeria bao 1-0,Tanzania walipata bao dakika ya 84 likiwekwa kimiani na Thomas Ulimwengu kwenye uwanja Taifa jijini Dar es salaam

Thursday, June 02, 2011

AJALI NYINGINE MBEYA


Basi la kampuni ya Abood jana lilianguka eneo la mlima nyoka na kujeruhi abiria 36,kwa bahati nzuri halikusababisha vifo kwa abiria wake,huu ni mfululizo wa ajali kutokea mkoani Mbeya,Ijumaa iliyopita basi la Sumry lilipata ajali na kupoteza maisha ya watu 13 na wengine kadhaa kujeruhiwa,Abood ilikuwa ikitokea Dar es salaam kuja Mbeya.

MAFUNZO YA UZIMAJI MOTO


Bw.Hashim Yahya Mbelwa akitoa elimu kwa wafanyakazi wa BTS jinsi ya kuzima na kukabiliana na moto kwenye ukumbi wa BTS semina hiyo ilikuwa nzuri na kueleweka na kila mmoja.

MAFUNZO YA UZIMAJI MOTO


Bw.Hashim Yahya Mbelwa akitoa elimu kwa wafanyakazi wa BTS jinsi ya kuzima na kukabiliana na moto kwenye ukumbi wa BTS semina hiyo ilikuwa nzuri na kueleweka na kila mmoja.

MAFUNZO YA KUZIMA MOTO


Bi Helen Kataraiya akifanya moja ya majaribio ya kuzima moto huku akisimamiwa na mmoja wa wakufunzi wa semina hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa BTS Mbeya,moto ni rafiki haumchokozi mtu mpaka ukosewe.

Tuesday, May 31, 2011

MSIBA


Mwili wa marehemu magreth Komba ukipakiwa kwenye gari tayari kwa mazishi yatakayofanyika eneo la Uyole Mbeya kabla ya kufanyiwa swala na viongozi wa dini.

Wauguzi na madaktari wa hospitali ya rufaa Mbeya, wakitoa heshima za mwisho kwa mtumishi mwenzao Magreth Komba pamoja na mumewe waliofariki kwa ajali ya basi.

Monday, May 30, 2011

MBEYA (MAPINDUZI STARS) WAPOKELEWA KWA VIFIJO NA NDEREMO.


Golikipa wa mkoa wa Mbeya Ivo Mapunda akimkabidhi kombe la ubingwa wa taifa mkuu wa mkoa wa Mbeya mh.John Mwakipesile leo katika hafla fupi ya kuwapokea mashujaa hao wa mkoa wa Mbeya mara baada ya kurejea kutoka Arusha-picha kwa hisani ya mbeya yetu blogspot.com

Mchezaji bora wa kombe la Taifa kwa mwaka 2011 Juma Mpola akiwa na daktari wa timu ya mkoa wa Mbeya wakiwa kwenye trela la TBL ambao ni wadhamini wa Kombe la Taifa kwa kupitia bia yao ya kilimanjaro

Sunday, May 29, 2011

BARCELONA BINGWA ULAYA


Timu ya Barcelona imetwaa ubingwa wa ulaya baada kuwachapa Manchester united bao 3-1,goli la kwanza la Barca liliwekwa kimiani na Pedro na Man walisawazisha kupitia Wayne Rooney hadi mapumziko timu hizo zilikuwa nguvu sawa,kipindi cha pili Barcelona walifanikiwa kupata mabao mawili kupitia kwa Leone Messi na David Villa mechi hiyo imechezwa kwenye uwanja wa Wembley jijini London.

Saturday, May 28, 2011

WYDAD CANSABLANCA YAICHAPA SIMBA 3-0.


Timu ya Simba leo imefungwa jumla ya mabao 3-0 na Wydad Cansablanca ya Morroco magoli ya wamorroco hao yamefungwa dakika ya 87 na mengine mawili yakifungwa dakika za majeruhi,mchezo huo umechezwa kwenye uwanja Petrosport jijini Cairo,na hivyo kuzima ndoto za Simba kucheza hatua ya makundi klabu bingwa Africa,sasa wataingia kwenye michuano ya kombe la shirikisho na kucheza na Motema Pembe ya Congo

MBEYA BINGWA KOMBE LA TAIFA


Timu ya mkoa wa Mbeya leo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe la taifa baada ya kuifunga timu ya mkoa wa Mwanza kwa bao 1-0,bao pekee la Mbeya limefungwa dakika ya 87 na mshambuliaji tishio nchini Gaudence Mwaikimba.

BASI LA TAQWA LAANGUKA.


Zaidi ya abiria 50 wamenusirika kifo baada ya basi la taqwa kuanguka eneo la Iyofi mpakani mwa mikoa ya Morogoro na Iringa,basi hilo lilikuwa likielekea jijini Dar es salaam.

SUMRY YAPATA AJALI MBAYA.


Basi la kampuni ya Sumry high class limepata ajali eneo la Igawa na kupoteza maisha ya abiria 13 na wengine kujeruhiwa,basi hilo lilipata ajali kutokana na kupasuka tairi la mbele na kusababisha basi hilo kupinduka,basi hilo lilikuwa likitokea jijini Arusha.

Wednesday, May 25, 2011

OBAMA ASEMA LAZIMA GADAFFI AONDOKE


Rais Barack Obama amesema lazima rais Muamar Gadaffi aondoke madarakani,ameyasema katika yake nchini Uingereza,nchi imekuwa na machafuko ya kisiasa kwa mitatu na zaidi,huku nchi za ulaya zikionekana kuwaunga mkono waasi wa serikali ya Libya.

MBEYA YAINGIA FAINALI KOMBE LA TAIFA


Timu ya mkoa wa Mbeya(Mapinduzi stars) imefanikiwa kuingia fainali ya michuano ya kombe la taifa,baada ya kuifunga timu ya mkoa wa Kagera kwa jumla ya mabao 2-1,mchezo huo umechezwa kwa dakika 120,hadi dakika 90 zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana 1-1,Mbeya ndio waliofanikiwa kupata ushindi baada ya beki wa Kagera kujifunga baada ya shambulizi kutokea golini kwao,mchezo huo ulikuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote kucheza soka maridadi na golikipa wa Mbeya Ivo Mapunda kuonyesha uwezo mkubwa,Mbeya watakutana na Mwanza Heroes siku ya jumamosi uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha katika fainali.

Thursday, May 19, 2011

SIMBA KUVAANA NA WYDAD CANSABLANCA CAIRO

Timu ya Simba imfanikiwa kurudi kwenye michuano ya klabu bingwa Africa baada ya rufaa yao kukubaliwa na shirikisho la soka Africa(CAF) na kuitupia mbali timu ya TP Mazembe ambao ndio mabingwa wa kombe hilo baada ya kumchezesha mlinzi halali wa timu ya Esperence ya Tunisia,sasa simba watacheza na wydad cansablanca ya Morocco kwenye uwanja huru huko jijini Cairo

AJALI MBAYA GEITA

Ajali mbaya imetokea Geita baada ya basi la sheraton kugongana na lori na kusababisha watu kumi na sita kupoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa

Sunday, May 15, 2011

AJALI


Gari kubwa aina ya scania likiwa limeacha njia na kujikita kwenye mitaro iliyopo pembeni ya barabara,eneo la Iwambi Mbeya.

Msongamano huu umesababishwa na lori liliacha njia na kujikita kwenye mtaro wa barabara eneo la Iwambi-Mbeya.

Thursday, May 12, 2011

MAMA NA MWANA

Mama Mchungaji wa kanisa la moravian usharika wa NZOVWE  mama Salome Kalengo,akiwa na watoto wake walipotembelea ofisini kwake

Sunday, May 08, 2011

MANCHESTER UTD YAICHAPA CHELSEA 2-0


Manchester utd imezidi kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa England baada ya kuwachapa Chelsea kwa bao 2-0,na hivyo kuwa mbele kwa pointi 6 na zikiwa zimebakiwa na mechi 2 nao Arsenal wamepokea kichapo cha bao 3-1 kutoka kwa Stoke City.

KOMBE LA TAIFA


Timu ya mkoa wa Rukwa imeweza kufanya maajabu kwa kuifunga timu ya mkoa wa Temeke kwa jumla ya bao 2-1,Rukwa walikuwa wa kwanza kupata goli kwa njia ya adhabu dakika 12 baadaye nao Temeke walisawazisha nao kwa njia ya adhabu,kipindi cha pili Rukwa walifanikiwa kupata bao la pili.Katika mchezo wa kwanza Mbeya walifanikiwa kuwafunga Iringa 2-1.

Thursday, May 05, 2011

WEMBLEY PATACHIMBIKA


Kocha wa manchester akishangilia ushindi dhidi ya Schalke 04 ya Ujerumani

MANCHESTER UTD USO KWA USO NA BARCELONA MEI 28

Wachezaji wa manchester united wakishangilia moja ya mabao waliopata jana kwenye mchezo wa klabu bingwa ulaya kati yake na SCHALKE 04,ambapo manchester walifanikiwa kupata ushindi wa mabao 4-1 na kusonga kwa jumla mabao 6-1,sasa watakutana na Barcelona katika mchezo wa fainali tarehe 28 mei,kwenye uwanja wa Wembley  England.

Wednesday, May 04, 2011

BARCELONA YATINGA FAINALI

Timu ya Barcelona jana ilifanikiwa kuingia fainali ya klabu bingwa ulaya baada ya kutoka sare na Real madrid 1-1,ilikuwa ni Barcelona iliyokuwa ya kwanza kujipatia lililofungwa Pedro dakika ya 56 madrid walisawazisha dakika ya 66 kupitia Marcus kwa matokeo hayo Barca wanaingia fainali na moja kati ya itakayoshinda leo kati Man utd v/s Schalke 04

SEHEMU ALIYOKUWA AKIISHI OSAMA BIN LADEN

Hii ndio nyumba aliyokuwa akiishi Osama bin Laden eneo la obbottabad nje kidogo ya jiji Islamabad Pakistan,ambayo ilishambuliwa na majasusi wa kimarekani na kufanikiwa kumuuwa kiongozi huyo wa kundi la al quaider

Monday, May 02, 2011

OSAMA BIN LADEN AUAWA PAKISTAN

Kiongozi wa kundi la al-queida ameuawa na wanajeshi wa Marekani waliokuwa wakifanya operesheni maalum nchini Pakistan,Osama bin laden amekuwa akisakwa kwa zaidi ya miaka kumi na moja sasa

Thursday, April 28, 2011

CHANGIA DAMU OKOA MAISHA


Waelimishaji kutoka kitengo cha taifa cha damu salama kanda ya nyanda za kusini,wakitoa elimu juu ya uchangiaji damu kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lwati wilayani Mbozi-Mbeya.Kwa kutumia blog hii nawapongeza wafanyakazi wa kitengo husika na wale wote wenye moyo wa kujitolea kwa ajili ya wahitaji-Amen.

ELIMU NA KAZI


Wanafunzi wa shule ya sekondari Lwati wilayani Mbozi,wakiwa kwenye shamba la migomba wakifanya kazi kwenye moja ya mashamba ya shule hiyo.

Sunday, April 24, 2011

PASAKA NJEMA


Bw.Benjamin J.Kaminyoge,anawatakia wakristo wote ulimwenguni heri ya sikukuu ya Pasaka,kwa kutumia sikukuu hii tusameane makosa yetu na kuwa na upendo.

MITAMBO YA KUPIMIA MITA ZA MAJI


Mdau wetu akiwa ametembelea mitambo maalumu inayotumika kupima mita za maji zenye matatizo huko Mbeya.

Sunday, April 17, 2011

MANCHESTER YAKABWA KOO


Manchester united jana imefungwa bao 1-0 na mahasimu wao Manchester City,katika michuano ya FA CUP,michuano hiyo imekuwa na msisimko mkubwa kwa timu ndogo kuzitoa jasho timu kubwa.

Saturday, April 16, 2011

AJALI MBAYA YATOKEA ARUSHA

Poleni ndugu zetu wa Arusha kwa msiba uliowapata  kutokana na ajali ya iliyohusisha basi la kampuni ya ngorika na basi dogo aina ya hiace na kusababisha vifo vya watu na wengine kujeruhiwa.

Thursday, April 14, 2011

SHITAMBALA AISALITI CHADEMA

Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha maendeleo mkoa wa Mbeya ameamua kuhama chama chake na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM,uamuzi wake umepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi mkoani Mbeya

Monday, April 11, 2011

YANGA BINGWA


Timu ya Yanga imetwaa ubingwa wa Tanzania bara baada ya kuifunga Toto African kwa jumla ya mabao 3-0,magoli ya Yanga yalifungwa na Nurdin Bakar na Davies Mwape yote kipindi cha pili,hivyo kuifanya Yanga kufikisha pointi 49 sawa na mahasimu wao Simba lakini wanakuwa mabingwa kwa tofauti ya magoli,Simba waliifunga Majimaji ya Songea bao 4-1.

Saturday, April 09, 2011

STENDI KUU MBEYA


Ukarabati unaoendelea ndani ya kituo cha mabasi Mbeya umesababisha lango la kutokea kufungwa kwa muda na kusababisha gari zote kuingia na kutokea mlango mmoja,imekuwa ni taabu hasa asubuhi zinapoondoka gari za mikoani.

Wanafunzi wakipata elimu kwenye ukumbi wa mikutano chini ya bwana Morgan Seben.

Wanafunzi wa Swaya sekondari wakipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa kitengo cha damu Mbeya bwana Morgan Seben walipotembelea kitengo hicho.


ZIARA YA WANAFUNZI WA SEKONDARI YA SWAYA-MBEYA.


Wanafunzi wa Swaya walipotembelea benki ya damu kwa ajili ya mafunzo juu ya mfumo wa damu.

Eneo la Kabwe Mbeya.

MVUA NDANI YA MBEYA


Baadhi ya mitaa jijini Mbeya imekuwa ni kero kutokana na mvua inayoendelea kunyesha na kusababisha barabara kujaa maji kutokana na mashimo kama inavyoonekana moja ya barabara eneo la Soweto.

YANGA YAKARIBIA UBINGWA


Timu ya Yanga imeamusha matumaini ya kutwaa ubingwa msimu huu baada ya kuwachapa African Lyon kwa jumla ya bao 3-0 na kufikisha pointi 46 na kubakiwa na mechi moja sawa na mahasimu wao Simba ambayo nayo imebakiza mchezo mmoja dhidi ya Majimaji.

Wednesday, April 06, 2011

SIMBA ALMANUSRA KWA RUVU JKT


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara Simba leo wamenusurika kichapo kutoka kwa maafande wa JKT RUVU baada ya kusawazisha bao kwa njia ya penati iliyofungwa na Emanuel Okwi,ilikuwa ni JKT RUVU iliyokuwa ya kwanza kujipatia bao la kuongoza kipindi cha kwanza lililowekwa kimiani na Hussein Bunu na kudumu hadi mapumziko,Simba ambao leo walionekana kubanwa vilivyo na wapinzani wao,mwamuzi wa mchezo huo alishindwa kuumudu mchezo huo na kuwatoa nje wachezaji wa JKT akiwemo Shabaan Dihile na George Minja,ligi hiyo itaendelea tena kesho kati ya Yanga dhidi ya African Lyon,Yanga wanahitaji ushindi ili kujiwekea mazingira mazuri ya kunyakua ubingwa.

VODACOM WABADILISHA RANGI YAO.


Linaloonekana ni jengo la Vodashop Mbeya,likiwa linaendelea kupigwa rangi tofauti na ile iliyozoeleka na wengi ya bluu sijui na jina litakuwaje?umekuwepo mchezo wa kubadili majina na rangi kwa baadhi ya makampuni ya simu kama vile mobitel wakaitwa Buzy na sasa tigo na Celtel wakaitwa Zain na sasa Airtel.