BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Monday, August 22, 2011

MAMBO YA KYELA

Hili ni eneo la Kyela mjini ambalo ni maarufu kwa uuzaji wa mchele safi na wanawake wenye uwezo mkubwa wa kuendesha baiskeli kwa umbali mrefu
Huu ni mkusanyiko wa baiskeli za wanafunzi waliopaki eneo la shule wilayani Kyela

 

wakina mama wakiwa na baiskeli zao




Sunday, August 21, 2011

MZIMU WA SIMBA WAENDELEA KUITAFUNA YANGA


Mabingwa wa Tanzania bara leo wameanza ligi ya Vodacom vibaya,baada ya kufungwa bao 1-0 na JKT Ruvu ikiwa ni siku chache baada ya kupokea kichapo kutoka kwa mahasimu wao Simba cha bao 2-0 kwenye mchezo wa ngao ya hisani,JKT Ruvu walipata bao kwa njia ya penati dakika 22 iliyofungwa na Kesy Mapande kutokana na mlinzi wa Yanga Chacha Marwa kucheza faulo eneo la hatari.
JKT Ruvu walitumia mbinu iliyotumiwa na Simba ya kuchezesha viungo wengi katikati na hivyo kuwafanya viungo wa Yanga Nurdin Bakari na Haruna Niyonzima kushindwa kuonyesha umahiri wao ipasavyo.
Na huko Arusha Simba wameanza ligi vyema baada ya kuwalaza JKT Oljoro mabao 2-0.

Saturday, August 20, 2011

SONGEA


Hapa ndio katikati ya mji wa Songea ambako kuna purukushani za hapa na pale na pikipiki za abiria nyingi

SONGEA ASUBUHI YA LEO


Mdau wetu akiwa kituo cha mabasi Songea tayari kwa safari.

Friday, August 19, 2011

USAFIRI WA LITEMBO-MBINGA


Kutokana na wilaya ya Mbinga kuwa na milima mingi wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakitumia usafiri wa Land Rover,ambazo zimepewa na kuitwa Mondolino kutokana na uwezo kupanda na kushuka milima hiyo huku zikiwa na abiria wengi na mizigo mingi.

UZALENDO KWA TAIFA LETU.


Majengo ya shule ya sekondari ya Kiamili Wilayani Mbinga,yakiwa yamepakwa rangi za bendera ya Taifa,hii ni moja ya uzalendo kwa taifa letu na kuwafanya hata wanafunzi kuelewa rangi za bendera hiyo kiurahisi zaidi.

MNYAMA AITAFUNA YANGA USIKU


Timu ya Simba imefanikiwa kuwafunga mahasimu wao Yanga kwa mabao 2-0 na kuchukua ngao ya hisani,Simba wakicheza kwa ushirikiano mkubwa walifanikiwa kupata bao dakika ya 16 kupitia Haruna Moshi Boban na baadaye walipata bao kwa njia ya penati kupitia kwa Sunzu hadi mapumziko Simba walikuwa wakiongoza kwa mabao hayo mawili,kipindi cha pili Simba waliingia kwa kasi na kuwafanya Yanga washindwe kusawazisha kutokana na kuwazidi wapinzani wao kwenye safu ya kiungo na kuwafanya Yanga kucheza bila malengo.
Timu hizi zimekutana mara sita kwenye mechi za usiku na hivyo Simba ikiibuka na ushindi mara tano na Yanga mara moja na mechi hizo zilichezwa uwanja wa Aman Zanzibar,mechi nne zikiwa ni za ubingwa wa Afrika mashariki na kati,moja kombe la muungano na nyingine ndio hii ya ngao ya hisani ambayo imechezwa uwanja wa Taifa Dar es salaam kwa matokeo hayo inaonyesha Yanga wamekuwa na udhaifu wa mechi za usiku hata za kirafiki,wiki moja tu iliyopita wamechezea kichapo mjini Khartoum Sudan kwa kufungwa mabao 3-1 na El-hilal,na katika mechi ya pili wakapokea kipigo kama hicho hicho
Mvuto zaidi ni kwa makocha wa timu hizo ambao wanatoka nchi moja kwa upande wa Simba ni Moses Basena na Yanga ni Sam Timbe ambao kila mmoja alitaka kuonyesha nani zaidi ya mwenzake kutokana na timu zote kujivunia usajili wa msimu huu.

Tuesday, August 16, 2011

CHANGIA DAMU OKOA MAISHA.


Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Agustivo High School wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma,wakiwa na mfanyakazi wa kitengo cha Taifa cha damu salama kanda ya nyanda za juu kusini bw.Fred Malagi wakati wa zoezi la kuchangia damu lililofanyika shuleni hapo mapema leo.

Sunday, August 14, 2011

MASHINDANO YA KUHIFADHI KURAAN TUKUFU YAFANA DAR


Baadhi ya mashekhe na umati wa waislamu uliofurika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee hall jijini Dar-es-salaam,kushuhudia mashindano ya kuhifadhi Kuraan Tukufu yaliyoshirikisha wanafunzi wa madrasa toka bara na visiwani,ambayo mshindi wa kwanza alikuwa Khalid Omar Mbarouk(15) kutoka madrasa ya Madrasat An-nujum ya Temeke na kujishindia pikipiki aina ya Bajaj.

UJENZI WA BARABARA YA SONGEA-MBINGA WAENDELEA KWA KASI.


Ujenzi wa barabara ya Songea-Mbinga kwa kiwango cha lami,unaendelea kwa kasi na kuleta matumaini kwa wakazi mkoa huo kutokana na wilaya ya Mbinga kuwa na vyanzo vingi vya mapato.
Kukamilika kwa ujenzi kutawanufaisha wakazi wa mkoa wa Ruvuma na maeneo jirani waliokuwa wakitumia muda mrefu kusafiri katika maeneo hayo yenye biashara za mazao na samaki kutoka ziwa Nyasa.

MANCHESTER YAANZA VIZURI


Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Uingereza (EPL) leo wameanza michuano hiyo vizuri baada ya kuwafunga timu ya West ham 2-1,Man walikuwa wa kwanza kupata bao dk 14 kupitia kwa Wayne Rooney na baadaye Long aliisawazishia Westham na kufanya matokeo kuwa 1-1 hadi mapumziko,kipindi cha pili Man walifanikiwa kupata bao la ushindi dk 81 kupitia kwa Ashley Young aliyepiga mpira na kuwababatiza mabeki wa Westham na kujaa wavuni

KITUO CHA MABASI NJOMBE VUMBI TUPU


Pamoja na uchumi mkubwa wa Njombe,kituo cha mabasi bado kinahitaji ukarabati wa hali juu na kufanya kiendane na hadhi ya wilaya hiyo ambayo inategemewa kupewa hadhi ya mkoa

Friday, August 12, 2011

KILIMO CHA KIANGAZI MBEYA


Kutokana na hali na hewa kuwa nzuri katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Mbeya,sehemu nyingine wanalima mahindi mara mbili kwa mwaka kama inavyoonekana eneo la Maganjo eneo la Mbeya vijijini

Thursday, August 11, 2011

UKOSEFU WA MAFUTA MBEYA WASABABISHA SHIDA YA USAFIRI


Kukosekana kwa mafuta kumesababisha watu kuchelewa maeneo yao ya kazi na wengine kulazimika kutembea kwa miguu,kutokana na baadhi ya daladala kushindwa kutoa huduma ipasavyo kutokana na vituo vya mafuta kuishiwa mafuta.

IGOMA MBEYA


Mdau wetu akiwa kwenye kijiji cha Igoma Mbeya,njia panda ya kuelekea wilaya ya Makete mkoani Iringa.

Wednesday, August 10, 2011

MACHAFUKO UINGEREZA YATIBUA MCHEZO WA TIMU YA TAIFA.


Machafuko yaliyokuwa yakiendelea nchini Uingereza yamesababisha mechi ya kirafiki kimataifa kati ya Uingereza na Uholanzi kufutwa na baadhi ya michezo ya kombe la Carling kuahirishwa.

Sunday, August 07, 2011

RAIS KIKWETE ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI.


Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,amemtumia salamu za rambirambi mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini,Jenerali Davis Mwamunyange.kufuatia kifo cha Luteni Jenerali Silas Peter Mayunga kilichotokea jana katika hospital ya Apollo,mjini New Dhel,India.Mzee Mayunga amefariki akiwa na umri wa miaka 71.

Saturday, August 06, 2011

BIASHARA YA NDIZI TUKUYU.


Wafanyabiashara ya ndizi wakionekana wakisubiri usafiri kwa ajili ya kusafirisha ndizi kupeleka maeneo tofauti,biashara hiyo inaonekana kufanywa na wanawake kuliko wanaume eneo la Tukuyu na hivyo kusababisha soko lake liwe dogo,kufunguliwa kwa uwanja wa ndege wa Songwe kutaleta changamoto kwa wanaume nao kujiingiza kwenye biashara hiyo ambayo wamekuwa kama wanahidharau.

Wednesday, August 03, 2011

MAJENGO YA ILIYOKUWA HOSPITAL YA UKOMA MAKETE-KISONDELA YAMETELEKEZWA TOKA 2005

Haya ni majengo ya iliyokuwa hospital ya ukoma  Makete Kisondela,Rungwe yakiwa kwenye hali mbaya baada ya hospital hiyo kufungwa rasmi mwaka 2005 na kufanya majengo kubaki yakiwa hayatumiki mpaka leo.
   Majengo haya yangeweza kutumika kama shule au kituo cha afya kwenye kata husika lakini yameachwa yakiharibika
Sehemu ya ndani ya majengo hayo ambayo haitumiki kwa sasa

Jengo likiwa limezungukwa na nyasi pande zote


WEST TEXAS LAKE


West Texas reservoir turns blood red,Thousands of dead fish float in a feew feet of dark red water that some are saying is a sign of end times.

Monday, August 01, 2011

RAMADHAN NJEMA


Tunawatakia mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhan waislam wote duniani,na kutenda mambo mema siku zote kama alivyoagiza mwenyezi Mungu.

Saturday, July 30, 2011

SUPER FEO YAPATA AJALI MBEYA

Basi la kampuni ya Super Feo limepata ajali la eneo Chimala Mbeya jana mchana na kusababisha vifo vya watu watatu na wengine kujeruhiwa,nilizungumza na mmoja wa majeruhi bw.Jackson Ndaskoy aliyekuwa akitokea Songea,alisema sababu ya ajali ni dereva kutokuwa makini bw.Ndaskoy ameruhusiwa kutoka hospilini mchana huu wa leo

Friday, July 29, 2011

KIONGOZI WA WAASI LIBYA AUAWA

Kiongozi wa waasi wa serikali ya Muamar Gadaffi bwana ABDEL fattah younes,ameuawa kwa kupigwa risasi mjini Tripoli,

TBL YAKABIDHI VIFAA YANGA NA SIMBA


Katibu mkuu wa shirikisho la soka nchini(TFF) Angetile Osiah akiongea wakati wa hafla hiyo


 
Viongozi wa Yanga na Simba wakionyesha vifaa walivyokabidhiwa na TBL

TUNDU LISSU,PETER MSIGWA NA GODBLESS LEMA WAFUKUZWA BUNGENI

Askari polisi wa bunge wakihakikisha gari lililowabeba wabunge wa CHADEMA Tundu Lissu ,Peter Msigwa na Godbless Lema linaondoka nje ya viwanja vya bunge mara baada ya naibu spika wa bunge Job Ndugai kuwaamuru watoke ndani ya bunge kutkana na kukiuka kanuni za bunge

Wednesday, July 27, 2011

MIKOA YENYE CHAKULA WATUMIE KWA UHANGALIFU

Hapa ni eneo la Kiwira Tukuyu Mbeya,ni eneo maarufu kwa uhuzaji wa ndizi,mananasi,magimbi nk.wanunuzi  wakubwa ni wasafiri waendao nchi jirani,nje ya mkoa na hata wilaya jirani,kutokana na tamaa ya fedha baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakiuza mpaka ndizi ambazo muda wake bado,pia tunawashauri kuwa waangalifu na uhuzaji holela wa vyakula kutokana na upungufu uliojitokeza kwenye baadhi ya mikoa na nchi jirani

MAPOROMOKO YA MAJI IBUNGILA TUKUYU YATUMIKA VIZURI


Maporomoko ya maji eneo la Ibungila Tukuyu yametumiwa vizuri na kuweza kuzalisha umeme kwenye shule ya sekondari Ibungila na maeneo jirani.



Mdau wetu alipotembelea eneo la maporomoko hayo

Hii ndio mashine ya kufua umeme Ibungila

Monday, July 25, 2011

SIKU YA MASHUJAA KITAIFA


Askari wa jeshi la wananchi wakitoa heshima kuwakumbuka mashujaa katika siku ya mashujaa.

Sunday, July 24, 2011

MAZISHI YA MZEE GILBERT MWAKIFULEFULE YAFANYIKA LEO IPINDA KYELA


Mazishi ya mzee Gilbert Mwakifulefule yamefanyika leo kijijini Ngolela,Ipinda-Kyela,askofu mkuu wa kanisa la kiinjili la Moravian amewataka waumini na waombolezaji kutengeneza maisha yao ya baadaye na upendo-

Wakina mama wakiwa kwenye majonzi

Saturday, July 23, 2011

BABU LOLIONDO ABADILI FANI


Kama kuna mtu ambaye ana ushawishi mkubwa kwa Afrika Mashariki huwezi kuacha kumtaja Mch.Mstaafu A.Mwaisapile,baada ya kupungua wagonjwa waliokuwa wakifika kwake sasa anaendelea kujenga nyumba yake yeye mwenyewe.

Thursday, July 21, 2011

NGASSA AOSHA NYOTA YAKE

Mshambuliaji wa Taifa stars anayechezea timu ya Seattle Sounders ya USA,akijaribu kumtoka mlinzi Fabio(kulia) wa Manchester United kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa nchini Marekani















WATU WANNE WAPOTEZA MAISHA AJALI YA BASI

Haya ndio mabaki ya basi la Hood lililopata ajali jana  na hatimaye kuungua baada ya kugongana na lori lililokuwa limepakia mafuta ya kula
Lori la mafuta likiteketea kwa moto eneo la Mikumi baada ya kugongana na Hood

MKUU WA MKOA WA MBEYA AKUTANA NA MADEREVA WA MAGARI MAKUBWA

Mkuu wa mkoa wa Mbeya mh. John Mwakipesile akifafanua jambo kuhusu kuongezeka siku za kukagua na kusimamia magari kwenye mizani iliyoko Mpemba-Tunduma-Picha kwa hisani ya Mbeya Yetu

Kamanda wa polisi wilaya ya Mbozi,afande Ernest Dudu nae alizungumzia utaratibu wa askari wa usalama barabarani kukagua magari hayo eneo la mizani

Wednesday, July 20, 2011

BREAKING NEEEEEWSSSS.


Habari zilizotufikia hivi punde kutoka kwa mwandishi wetu aliyeko Morogoro ni kuwa basi lililokuwa likisafiri kati ya Mbeya na Arusha limeshika moto eneo la Mikumi na abiria kushindwa kuendelea na safari,basi hilo ni mali ya Hood transport ya Morogoro
Basi likiendelea kuwaka moto

MRISHO NGASA AKIWA MAZOEZINI MAREKANI


Mshambuliaji maarufu wa Taifa stars na Azam fc,akiwa kwenye mazoezi na wenzake kwa ajili ya kuwakabili mabingwa EPL timu ya Manchester United ya Uingereza,Ngassa aliyeonyesha uwezo mkubwa akiwa na Yanga SC misimu iliyopita na hivyo kuwavutia Azam na kumchukua kwa dau kubwa,kwa sasa anafanya majaribio kwenye klabu ya Seattle Sounders ya Marekani na anaendelea vizuri.

Tuesday, July 19, 2011

TERRY-MODRIC 'DISRESPECTFUL'


John Terry believes Luka Modric has been disrespectful to Spurs for trying to engineer a move to Stamford Bridge.

Monday, July 18, 2011

VODACOM NA MRADI WA UTUNZAJI WA MBWA MWITU SERENGETI

Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania bw.Dietlof Mare akimkabidhi sanamu ya mbwa mwitu mkurugenzi wa shirika la hifadhi ya Taifa TANAPA,Allan Kijazzi kama ishara ya uzinduzi rasmi wa mradi wautunzaji mbwa mwitu katika hifadhi ya tafa Serengeti(Vodacom foundation's Serengeti wild dogs conservation project)
Mkurugenzi mkuu wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare akiteta jambo na waziri wa mawasiliano na uchukuzi mh.Mahige

Sunday, July 17, 2011

MBEYA


Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya ndg.Advocate Nyombi akionyesha silaha iliyotumika kwenye uporaji wa fedha NMB-tawi la Kyela mkoani Mbeya.

Tuesday, July 12, 2011

LADY JAY DEE NA YANGA KESHO NYUMBANI LOUNGE.


Mwanamuziki maarufu ukanda huu wa afrika mashariki na kati,Judith Wambura (lady jay dee) amewaandalia chakula mabingwa wa Kombe la Kagame Castle Cup,timu ya Yanga chakula cha mchana kwenye mgahawa wake maarufu wa NYUMBANI LOUNGE kwa ajili ya kuwapongeza kwa kutwaa ubingwa,inasemekana mwanamuziki ni mnazi wa wanajangwani hao