BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, August 30, 2014

YANGA YATANGAZA KAMATI YA NIDHAMU,MAADILI NA SHERIA.

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA –(Utawala Bora) anapenda kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari kwa wana YANGA,ameunda Kamati ndogo chini ya Kamati ya Utendaji wa YANGA zifuatazo:
1) KAMATI YA MAADILI Wajumbe:   1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate) 2) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate)  3) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate) 4) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate) 5) Tenga, Cathbert (Advocate)
 2) KAMATI YA NIDHAMU Wajumbe:
  1) Karua, Tedy  2) Lamlembe, Roger 3) Kihanga, Pascal  4) Mahenge, Burton Yesaya 5) Mudhihir, Mudhihir (Advocate) 3)
 KAMATI YA SHERIA NA KATIBA  Wajumbe:
   1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate) 2) Gikas, Farija (Advocate) 3) Kabisa, Jessica (Advocate) 4) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate)  5) Kambamwene, January (Advocate) 6) Lupogo, Herman (Advocate) 7) Madibi, Richard (Advocate) 8) Mahenge, Burton Yesaya 9) Mgongolwa, Alex (Advocate) 10) Mkucha, Elisha (Advocate) 11) Mudhihir, Mudhihir (Advocate) 12) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate) 13) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate) 14) Tenga, Cathbert (Advocate) 15) Tenga, Ringo Dr. (Advocate) 16) Vedasto, Audax (Advocate 4)
 KAMATI YA UCHAGUZI Wajumbe:
  1)  Kajole, Mustafa  2)  Lundenga, Hashim Ibrahim  3)  Makele, Bakili  4)  Mlelwa, Daniel    5) Ngongolwa, Alex (Advocate) Ifahamike kwamba, kutakuwa na nyongeza ya uteuzi wa Wajumbe wengine wa Kamati za YANGA zilizotajwa hapo juu. Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA – (Utawala Bora) atakuwa Mwenyekiti wa Kamati zilizotajwa hapo juu. Kamati ya Utendaji ya YANGA, ina karibisha Wajumbe waliotajwa katika Kamati zilizotajwa hapo juu kwa dhamira njema kuwa watasaidia kujenga YANGA bora, na wanaomba ushirikiano kutoka kwa wanaYanga wote ili Wajumbe walioteuliwa waweze kutenda kazi zao vyema kwa manufaa ya YANGA. (YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO) (BENO NJOVU) KATIBU MKUU WA YANGA

Friday, August 29, 2014

AJALI KUBWA YATOKEA MBALIZI MBEYA

 Wimbi la ajali limezidi kulikumba jiji la Mbeya baada ya leo kutokea ajali eneo la Mbalizi na kugharimu maisha ya watu wasiopungua kumi na wengine zaidi ya sita wakijeruhiwa.
 Ajali hiyo imehusisha gari ya abiria(daladala) na lori dogo aina ya TATA, na kuleta simanzi kubwa kwa wakazi wa Mbalizi na maeneo ya jirani.
Wananchi wa Mbalizi wakiwa wamepigwa butwaa baada ya ajali iliyosababisha vifo vya watu.

Sunday, August 24, 2014

EL-MERREIKH MABINGWA AFRIKA MASHARIKI NA KATI 2014

  Timu ya El-merreikh ya Sudan imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Afrika mashariki na kati kwa kuwafunga APR ya Rwanda kwa bao 1-0,bao pekee la El-merreikh limefungwa na Allan Wanga dakika ya 25 ya mchezo na kuwafanya APR kushindwa kufurukuta mbele ya mashabiki wao na kunyang'anywa tonge mdomoni na wasudan hao.
  Mechi ya kutafuta mshindi wa tatu ilichezwa mapema na Police Rwanda wamepata nafasi hiyo kwa kuitoa KCCA ya Uganda kwa penati 4-2.

Wachezaji wa El-merreikh wakishangilia ushindi dhidi ya APR.

Tuesday, August 19, 2014

BIOGESI KWA MAISHA BORA

 Biogesi ni nishati itokanayo na kinyesi cha wanyama ambacho huchachuka ndani ya mtambo wa biogesi na kuweza kutumika kwa kupikia na kuwasha taa.
  FAIDA ZA BIOGESI:- .Haina moshi wala harufu mbaya
. Hupunguza madhara yanayosababishwa na moshi wa kuni au mkaa kama vile macho kuwa mekundu na kukohoa.
 .Huokoa muda Hupunguza muda wa kutafuta kuni hivyo kufanya shughuli nyingine za maendeleo.
 Mtandao huu umekutana na mtaalamu wa kutengeneza mtambo wa biogesi maeneo ya Mbinga Kigonsela bw.Linus Komba na kuelezea jinsi mtambo huu ulivyo rafiki wa mazingira,na kuwataka wananchi wa Tanzania hususani wale wanaoishi vijijini kuwasiliana naye ili aweze kuwasaidia na kuwafanya waendelee kuyatunza mazingira kwa kutokata miti,mnaweza kuwasiliana naye kwa simu yake ya mkononi +255 762 045 808,unaweza kuwasiliana naye na yuko tayari kuwafikia sehemu yeyote kwa ajili ya ushauri na matengenezo YATUNZE MAZINGIRA ILI UWAACHIE VIZAZI VIJAVYO SEHEMU NZURI YA KUISHI
Huu ndio mtambo wa biogesi ukiendelea kujengwa
Bw.Benjamin James akipata maelekezo kutoka kwa mafundi
Bw.Linus Komba akitoa maelezo kuhusu mtambo wa biogesi
Mafundi wakiendelea na kazi ya kukamilisha mtambo huo.

Sunday, August 17, 2014

MANCHESTER UNITED YAANZA VIBAYA EPL,YAPIGWA NYUMBANI

Ligi kuu ya Uingereza imefunguliwa huku matokeo yakiiduwaza Manchester United baada ya kukubali kichapo cha bao 2-1 wakiwa nyumbani,matokeo ambayo hawajawahi kuyapata kwenye mechi za ufunguzi toka mwaka 1972.
Matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:-
Man United 1-Swansea City 2 West Brom 2-Sunderland 2 Stoke City 0 -Aston Villa 1 Leicester City 2 Final Everton 2 QPR 0-Hull City 1 West Ham 0 -Tottenham 1 Arsenal 2-Crystal Palace 1 Sunday, August 17 Liverpool 3:30 PM Southampton Newcastle 6:00 PM Man City Monday, August 18 Burnley FC 10:00 PM Chelsea Saturday, August 23 Aston Villa 2:45 PM Newcastle Chelsea 5:00 PM Leicester City Swansea City 5:00 PM Burnley FC Crystal Palace 5:00 PM West Ham Southampton 5:00 PM West Brom Everton 7:30 PM Arsenal Sunday, August 24 Hull City 3:30 PM Stoke City Tottenham 3:30 PM QPR Sunderland 6:00 PM Man United Monday, August 25 Man City 10:00 PM Liverpool All times are in East Africa Time

Wednesday, August 13, 2014

REAL MADRID YATWAA EUROPEAN SUPER CUP

Ronaldo akishangilia moja ya gola lake


Mabingwa wa kihistoria wa UEFA CHAMPION LEAGUE,Real Madrid wamefanikiwa kuongeza kikombe kingine kwenye maktaba yao baada ya kuifunga Sevilla ya Spain bao 2-0 kwenye mchezo uliofanyika uwanja wa Cardiff,mabao ya Real Madrid yakifungwa na mchezaji hatari Christiano Ronaldo dakika ya 30 na 49.
  Sevilla walikuwa kama timu iliyokata tamaa kabla ya kuingia uwanjani kutokana na Real Madrid kuwa na washambuliaji wenye gharama kubwa na uwezo mkubwa uwanjani kama Gareth Bale,James,Kloose

Ronaldo na wenzake wakifurahia ushindi

Sunday, August 10, 2014

MAONESHO YA KILIMO KUFANYIKA MJINI NI KUMNYIMA MKULIMA ELIMU NA MAARIFA YA KILIMO.

 Wakulima wa mazao mbalimbali wamekuwa hawapatiwi elimu juu ya uzalishaji wa mazao yao,na hivyo kulazimika kufanya kilimo cha mazoea na kujikuta wakiendelea kupata mavuno kidogo.
Pia kufanyika maonesho ya kilimo maeneo ya mjini kila mara ni kumnyima mkulima maarifa zaidi ya kilimo.
Ikiwa maonesho haya yakiwa yanafanyika vijijini yanaweza kuwafanya wakulima kubadilishana ujuzi na kujifunza mambo mengi zaidi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu,kuliko kufanyika kila wakati mjini na kuyafanya kuwa ya kibiashara zaidi na kutembelewa na watu wasiokuwa walengwa na kuwaacha wakulima wakibaki vijijini kwa kunywa pombe na kucheza ngoma na kuona hiyo ndio furaha ya sikukuu ya wakulima.

Shamba la miti lililoko Vwawa Mbozi
Ndizi zikiwa zimeandaliwa kwa ajili ya kusafirishwa huko Ushirika Tukuyu

Moja ya shamba la mpunga wilayani Kyela
Kakao wilayani Kyela
Shamba la mahindi Ruanda Mbozi.
Shamba la miparachichi Itipingi Njombe.

KAGAME CUP 2014

Gor Mahia FC 1-2 KCC FC KCC FC opened their 2014 Kagame Cup campaign with victory after coming from a goal down to beat KPL champions Gor Mahia 2-1in the second of the day’s game played at Amahoro stadium. Uganda Cranes striker Daniel ‘Mzee’ Sserunkuma gave the Kenyan champions a deserved lead in the 27th minute before substitute Brian Majwega equalised for the Ugandan champions seven minutes after recess and later Umony netted the winner in the 88th minute. Gor Mahia started the brighter side and dominated proceedings launching numerous attacks on the KCC FC goal but goalie Yasin Mugabi was up to the task whenever called upon. Bobby Williamson’s charges however got a deserved lead after Musa Muhammad beat Namwanja Simon down the left to cross for Sserunkuma who tapped home despite a forest of legs inside the 18 yard area. The goal saw KCC FC coach George ‘Best’ Nsimbe react by substituting in the inefficient Steven Bengo for Brian Majwega but the Kenyan champions held on to their first half lead in a dominant display. After recess, Nsimbe made another change bringing on Brian Umony for Herman Wasswa. The Ugandan side started to dominate the game at this time and deservedly equalised through Majwega tapping home a fine cross from Tom Masiko. The Ugandan side was in ascendency at the moment but couldn’t break a resilient Gor backline manned by David Owino. At the other end, Gor Mahia threatened with Sserunkuma and later Timothy Otieno forcing a double save from Yasin Mugabi. With two minutes left on the clock, Brian Majwega broke down the left on a counter move and his low cross met Umony who slid the ball at the far corner past Onyango for KCC FC’s winner. KCC FC now top group B with maximum points and return to action on Sunday against Atletico at Nyamirambo. Last modified onFriday, 08 August 2014 18:34 200

Friday, August 08, 2014

YANGA KUTOSHIRIKI KAGAME CUP KUTAPOTEZA WAPENZI WAPYA WA NDANI NA NJE YA TANZANIA

 Yanga ni moja ya timu kubwa ukanda huu wa Afrika mashariki na kati na pengine ndio inaweza ikawa timu yenye washabiki wengi kwa ukanda huu wa Afrika mashariki.
 Kitendo cha timu hii kuwa matatizo ya maramara na shirikisho la soka la Afrika mashariki na kati(CECAFA) na kuifanya timu hii kuondolewa kushiriki michuano ya kombe la Kagame,kuna uwezekano mkubwa wa timu kupoteza wapenzi wapya kwa sababu hamna mtu anayependa kujiingiza kwenye kitu ambacho kina matatizo kila mara,na athari zake haziwezi kuonekana leo hii inaweza ikaonekana miaka ishirini ijayo au zaidi,kwa sababu wapenzi wapya ni wale ambao wana umri wa miaka mitano hadi kumi.
Wakisherekea ubingwa
Kikosi cha Yanga

Tuesday, January 14, 2014

CHRISTIAN RONALDO MCHEZAJI BORA 2014


Christian Ronaldo leo amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa dunia kwa mwaka 2014/15 kwa kuwashinda wachezaji Leon Messi wa Argentina na klabu ya Barcelona na Frank Ribery wa Ufaransa na klabu ya Bayern Munich.
Tuzo hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Leon Mess kwa miaka minne mfululizo.

KCC FC MABINGWA MAPINDUZI CUP 2014


Timu ya KCC ya Uganda leo imechukua ubingwa wa kombe la mapinduzi Zanzibar baada ya kuifunga timu ya Simba ya Dar es salaam kwa goli 1-0,kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Amaan,mjini Zanzibar,goli pekee la KCC limefungwa na Herman Waswa dakika ya 20.
 Kwa matokeo hayo timu ya KCC inakuwa timu ya kwanza kutoka nje ya nchi kuchukua ubingwa huo,mashindano yalikosa msisimko baada ya timu ya Yanga kujitoa dakika za mwisho na hivyo kuwakatisha tamaa wapenzi wa soka wa Zanzibar.
KCC waliingia fainali baada ya kuwachapa Azam 3-2 na Simba waliingia fainali kwa kuwachapa URA ya Uganda 2-0.

Sunday, May 19, 2013

YANGA BINGWA TANZANIA BARA


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati timu ya Yanga imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara ya 24 tangu ligi ihanzishwe 1965 kwa kuwafunga watani wao wa jadi Simba kwa goli 2-0.
Magoli ya mabingwa hao yalifungwa na Didier Kavumbagu dk ya 5 huku la pili likifungwa na Hamis Kiiza dk ya 63,Yanga walitawala sehemu kubwa ya mchezo huo na kushangiliwa kwa muda wote na mashabiki wake.
Simba walikosa penati dk ya 26 iliyopigwa na Mussa Mude lakini kwa umahiri wa kipa Ally Mustapha aliweza kuidaka penati hiyo.Sasa Yanga italikilisha Taifa kwenye michezo ya klabu bingwa Afrika na mshindi wa pili Azam atashiriki kombe la shirikisho Afrika.

Saturday, May 04, 2013

AZAM YAFA KISHUJAA MOROCCO


Wawakilishi pekee wa Tanzania waliokuwa wamebaki kwenye michuano ya kimataifa,timu ya AZAM FC leo wametolewa na AS FAR RABAAT ya Morocco kwa kufungwa 2-1 kwenye mchezo wa kombe la shirikisho uliochezwa nchini Morocco.
Azam walipata bao la kuongoza dakika ya 6 likifungwa na John Bocco na Far Rabaat walifanikiwa kusawazisha dakika ya 12 na kupata goli la pili dakika ya 43,dakika za mwisho wa mchezo Azam waliweza kupata penati lakini bahati haikuwa yao baada ya penati yao kugonga mwamba penati ilipigwa na John Bocco.
Mwamuzi alitoa kadi nyekundu tatu,moja kwa Far Rabaat na mbili kwa Azam, wadau wa soka wameisifu Azam kwa kuwa na maandalizi mazuri ya michuano ya kimataifa na kutegemea msimu ujao kufanya vizuri zaidi hii ni mara yao ya kwanza kushiriki michuano mikubwa kama hii.

Thursday, May 02, 2013

BARCELONA ULIMI NJE KWA BAYERN MUNICH YAPIGWA GOLI 7-0 KWA WIKI MOJA.


Timu ya Barcelona jana imepokea kipigo cha goli 3-0 nyumbani kutoka Bayern Munich na kutolewa kwenye nusu fainali na wajerumani hao
Mchezo wa kwanza uliochezwa Alienz Arena wiki moja iliyopita Barcelona walifungwa goli 4-0.
Bayern Munich sasa watakutana na wajerumani wenzao wa Borussia Dortmund kwenye mchezo wa fainali utaofanyika uwanja wa Wembly nchini Uingereza.

Saturday, April 27, 2013

BARCELONA NA REAL MADRID UGONJWA MMOJA WAPIGWA NNE NNE NA WAJERUMANI.


Real Madrid chini ya special coacher Jose Maurinho jana imepata kipigo kikubwa kutoka kwa Borussia Dortmund cha goli 4-1,kwenye nusu fainali ya klabu bingwa Ulaya.
Magoli ya Dortmund yote yamefungwa na Robert Lewandoski huku goli la kufutia machozi la Real Madrid likifungwa na Christian Ronaldo
Nao Barcelona juzi walikutana na kipigo kama hicho cha goli 4-0,kutoka kwa Bayern Munich,mechi za marudiano zitachezwa tarehe 30 na 31/05/2013 nchini Hispania.

Thursday, April 18, 2013

BI.KIDUDE AFARIKI DUNIA


Msanii mkongwe hapa nchini Fatma Baraka (Bi.Kidude) amefariki na atazikwa leo huko kijijini kwao Katumba Unguja.
Bi.Kidude alikuwa ni muimbaji wa nyimbo za taarab na mpiga ngoma maarufu,ambaye alikuwa maarufu ndani na nje ya nchi alikuwa kipenzi cha watu wengi kutokana na uwezo wake wa kulishambulia jukwaa pamoja na umri wake kuwa mkubwa.

Thursday, April 04, 2013

CANAAN HIGH SCHOOL-MLOWO MBOZI.


Ni moja ya shule nzuri zilizopo wilayani Mbozi,shule ipo eneo la Mlowo kilomita 1.2 toka barabara kuu iendayo Tunduma,shule ina walimu wazuri kwa masomo yote na mazingira mazuri kwa wanafunzi.
Pia ina Hosteli kwa ajili ya wavulana na wasichana,inapokea wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali,wahi sasa ili hupate nafasi kwenye shule hii yenye ubora mkubwa.

Thursday, March 28, 2013

EASTER CONFERENCE YAFANA MBEYA


Baadhi ya wanafunzi wa umoja wa wanafunzi wa kikristo Tanzania-Mkoani Mbeya wakimusikiliza Mhubiri toka Dar es salaam ndg.Jackson Mndeme kwenye mkutano unaofanyika kwenye ukumbi wa St.Mary's sekondari jijini Mbeya.

Monday, March 25, 2013

TAIFA STARS YAICHINJA MOROCCO 3-1


Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars jana imefanikiwa kuifunga kigogo cha soka Afrika Morocco bao 3-1 kwenye mchezo uliofanyika jijini Dar es salaam jana.
Taifa Stars walipata mabao yao kipindi cha pili yakifungwa na Thomas Ulimwengu na Mbwana Samata wanaochezea TP Mazembe ya DRC,sasa Stars inashika nafasi ya pili kwenye kundi lake ikiwa na pointi 6 nyuma ya Ivory Coast wenye pointi 7,Morocco ya tatu ikiwa na pointi 2,huku Gambia ikiburuza mkia.

Saturday, March 16, 2013

WASABATO MBEYA WAJITOKEZA KUCHANGIA DAMU.


Leo ilikuwa ya matendo ya huruma duniani kwa Wasabato na kukusanyika sehemu mbalimbali duniani kwa ajili ya kutoa elimu kwa watu juu ya ubaya wa matumizi ya Madawa ya kulevya,tumbaku na pombe.
Mbali na yote hayo Wasabato wa Mbeya Mjini walichukua nafasi hiyo kuchangia damu kwenye viwanja maarufu vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya,mmoja wa wachangiaji damu hao bw.Leonard Msendo alionekana kufurahia huduma ya uchangiaji wa damu na kuwaomba Watanzania kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wahitataji wa damu(wagonjwa) kwani damu ni tiba ambayo inapatikana kutoka kwa binadamu.
CHANGIA DAMU OKOA MAISHA-DAMU HAIUZWI HUTOLEWA BURE NA HOSPITALI ZOTE HAPA NCHINI,UKIUZIWA DAMU TOA TAARIFA KITUO CHA POLISI,MGANGA MKUU WA HOSPITALI HUSIKA AU KITUO CHA DAMU SALAMA KILICHO JIRANI NAWE.

Thursday, March 14, 2013

PAPA MPYA ATOKA ARGENTINA


 Hatimaye lile zoezi la kumchagua Papa limekamilika katika kanisa la St.Peters Basilica huko Vatican na Muargentina Jorge Mario Bergogli kuchaguliwa kuwa Papa mpya ambaye atajulikana kwa jina la PAPA FRANCIS WA KWANZA.

Sunday, March 10, 2013

SIMBA YAAMUKA USINGIZINI LEO KWA KUICHAPA COASTAL UNION 2-1


Mabingwa watetezi wa vodacom leo wamezinduka na kuichapa Coastal Union ya Tanga bao 2-1 kwenye uwanja wa Taifa Dsm.
Simba wamepata mabao ya mwishoni mwa kipindi cha kwanza kupitia kwa Mrisho Ngasa na Haruna Chanongo huku goli la kufutia machozi la Coast likifungwa na Razaq Khalfan kipindi cha pili.
Kwa matokeo hayo Simba kafikisha pointi 34 akiwa nyuma ya Azam wenye 37,huku vinara wa ligi hiyo Yanga wakiwa na pointi 45 na Coastal Union wanabaki na pointi 31 na kufanya ligi iwe ngumu kwa Azam,Simba na Coastal Union kwa mtazamo wangu Yanga hawana ugumu sana kwani wana uhakika wa nafasi moja kati ya tatu za juu,labda itokee walewe sifa na kupoteza takribani mechi nne ndio watakuwa pabaya.

YANGA YAWAADHIBU TOTO YAO


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga ya Dar es salaam imezidi kuisukumia kwenye shimo la kushuka daraja baada ya kuifunga bao 1-0 kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa.
Yanga walipata goli lao kupitia kwa Nizar Khalfan dakika 78,aliyeingia kuchukua nafasi ya Tegete.

Wednesday, March 06, 2013

RAIS HUGO CHAVEZ WA VENEZUELA AFARIKI DUNIA

Rais Hugo Chavez wa Venezuela amefariki jana,Rais Chavez alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kansa  ambayo yamesababisha kifo chake.
  Rais huyo atakumbukwa kutokana msimamo wake wa kutoyumbishwa na  baadhi ya mataifa yenye nguvu duniani

Saturday, March 02, 2013

MANCHESTER UNITED YAMUONGEZEA MKATABA RYAN GIGGS


Mchezaji mkongwe katika ligi ya Uingereza ameongezewa mkataba wa mwaka mmoja na klabu yake ya Manchester United.
Mchezaji huyo ambaye anatarajiwa kutimiza miaka 40 hivi karibuni utakuwa ni msimu wake wa 23 ndani ya Manchester united ni mmoja kati ya wachezaji waliyoipatia mafanikio klabu hiyo ya mashetani wekundu.

Monday, February 25, 2013

MZIMU WA LIBOLO WAENDELEA KUITESA SIMBA.











Mabingwa watetezi wa Tanzania Bara jana walizidi kupoteza matumaini ya kutetea ubingwa wao baada ya kufungwa na Mtibwa ya Morogoro kwa goli 1-0 kwenye uwanja wa Taifa Dar es salaam.
Mtibwa walipata bao lao dakika ya 18 likifungwa na Salvatory Ntebe akiunganisha pasi ya Vincent Barnabas,Simba imekuwa kwenye wakati mgumu toka walipomuuza nyota Emanuel Okwi na kumfukuza kocha wao Milovan Circovic na kuwafanya kuwa na matokeo yasiyoridhisha.

Tuesday, February 12, 2013

PAPA BENEDICT XVI ATANGAZA KUJIUZULU


Papa Benedict wa 16 ameushitua ulimwengu baada ya kueleza dhamira yake ya kutaka ifikapo februali 28 mwaka huu.
Kumekuwa na minong'ono mingi kutoka kwa baadhi ya watu wakidhani sasa umefika muda wa kanisa kuwa na mpasuko.

NIGERIA BINGWA KOMBE LA AFRIKA


Timu ya Taifa ya Nigeria imechukua ubingwa wa Afrika kwa kuichapa Burkina Faso goli 1-0,goli pekee la Nigeria limefungwa na Sunday Mba.

Saturday, February 02, 2013

YANGA YAPONEA KWENYE TUNDU LA SINDANO


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga leo wameponea chupuchupu kupoteza mchezo wa ligi kuu baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar
Mtibwa walipata bao la kuongoza dakika ya 45 likifungwa na Shaban Kisiga,Yanga wamefanikiwa kusawazisha dakika ya 85 kupitia kwa Hamis Kiiza ambaye aliunganisha mpira wa Said Bahanuzi.

Sunday, January 27, 2013

SIMBA YAANZA VIZURI MZUNGUKO WA PILI


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara jana wameanza vyema mzunguko wa pili wa ligi baada ya kuwachapa African Lyon goli 3-1,nao Azam FC wamepata ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Kagera Sugar,Mtibwa wameangukia pua baada ya kuchapwa goli 1-0 na Polisi Morogoro,Coastal Union wameibamiza JKT Mgambo 3-1,Toto African wamekubali kichapo toka kwa JKT Oljoro.
Ligi hii inaendelea leo kwa mchezo mmoja kati ya mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga na Tanzania Prison kwenye uwanja wa Taifa Dar es salaam.

Saturday, January 26, 2013

CHANGIA DAMU OKOA MAISHA


Mmoja wa washiriki wa Bonanza lililoandaliwa na Life time Promotion bw.Jafar Ngalipa akichangia damu kwenye viwanja vya TIA

Wednesday, January 09, 2013

YANGA YAPIGWA 2-1 UTURUKI


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga,jana wamefungwa goli 2-1 na timu ya daraja la kwanza nchini Uturuki ya Denizlispor.
Yanga wako nchini Uturuki ambako wameweka kambi ya wiki mbili.

Tuesday, January 08, 2013

YANGA UWANJANI TENA LEO


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga ya Dar es salaam,leo wanashuka tena dimbani kucheza na timu ya Denizlspor nchini Uturuki ambako Yanga wameweka kambi.
Yanga ikiwa imesheheni vipaji iliweza kupata matokeo ya sare ya 0-0 kwenye mechi yake ya kwanza na kuzivutia timu nyingine za nchi hiyo kutaka kucheza nayo.

Friday, January 04, 2013

DEREVA WA PIKIPIKI ANUSURIKA


Dereva wa pikipiki akiwa ahamini kilichotokea baada ya kunusurika kwenye ajali eneo la Kabwe Mbeya.

Tuesday, January 01, 2013

USIKU WA MWAKA MPYA 2013 VITUKO VITUPU.


Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Willy ameonekana akiwa amevaa suti iliyoshonwa kwa kutumia mifuko ya cement na kuvinjari mitaani maeneo ya Simike jijini Mbeya.
Ilikuwa moja ya burudani kwa wakazi wa eneo hilo la Simike.

KHERI YA MWAKA MPYA 2013


Mtandao huu unawatakia kila la kheri ya Mwaka mpya wasomaji wake wote,tumshukuru Mungu kwa kuweza kuufikia mwaka huu mpya na kutuepusha na mabaya mengi yaliyokuwepo na sasa tunaanza tena mwaka kwa kujikabidhi mikononi mwake.

Sunday, December 30, 2012

TUSKER FC YAICHAPA SIMBA 3-0


Timu ya Tusker FC ya Kenya,imeendeleza ubabe wake kwa timu za Tanzania baada ya kuichapa Simba kwa goli 3-0,kwenye mechi ya kirafiki iliyofanyika uwanja wa Taifa Dar es salaam.
Jumatano iliyopita waliwafunga mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga 1-0.

Sunday, December 23, 2012

TAIFA STARS YAWACHAPA MABINGWA WA AFRIKA


Timu ya Taifa ya mpira wa miguu Taifa Stars imewalaza mabingwa wa soka wa Afrika Zambia(Chipolopolo) goli 1-0 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es salaam.
Goli pekee la Taifa Stars lilifungwa na Mrisho Ngassa dakika ya 45 huku Zambia wakiwatumia wachezaji wao makini kama Christopher Katongo,Felix Katongo na Nathan Sinkala lakini hawakuweza kubadili matokeo.

Saturday, December 01, 2012

WATOTO WAPATA KIPA IMARA


Baadhi ya waumini wa kanisa la Moravian Mlowo wamepata kipa imara,kama wanavyoonekana watoto hao katika picha Noel Ben Kaminyoge,Rehema Mbuba wakiwa na wenzao ndani ya kanisa la Moravian Mlowo.

MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI-MBEYA.


Mamia ya wakazi wa Mbozi Mission wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Mh.Abbas Kandoro ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ambayo yamefanyika kimkoa wilayani Mbozi.
Mh.Kandoro amewaasa wananchi kuepukana na tabia hatarishi na kutowanyanyapaa wagonjwa wa ukimwi.
Mh.Kandoro aliwaongoza wananchi katika zoezi la kuchangia damu kwa hiari,baada ya kuchangia damu siku ya leo kwenye viwanja vya Mbozi Mission.

Thursday, November 29, 2012

ZANZIBAR HEROES YAWASHANGAZA AMAVUBI YAWACHAPA 2-1.


Timu ya Zanzibar leo imeweza kufanya kile ambacho hakikutegemewa na wengi baada ya kuifunga timu ngumu ya Ruanda(Amavubi) baada ya kuifunga goli 2-1 na kuingia robo fainali ya kombe la Tusker Challenge Cup.
Katika mechi ya kwanza Malawi wameibuka kidedea kwa kuwafunga Eriterea 3-2.