BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, May 20, 2012

TIMU YA STENDI KUU MBEYA YAICHAPA ITIJI RANGERS


Mashabiki wa timu ya stendi kuu Mbeya wakishangilia ushindi waliopata dhidi ya Itiji Rangers wa mabao 2-0,kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa shule ya msingi Mbata jijini Mbeya,mabao ya stendi kuu yamefungwa na Aliko Sanga na Dominick Meshack,hata hivyo mchezo uliingia dosari na mwamuzi aliamua kuvunja mchezo kutokana na Itiji kugomea mchezo.
Michuano hiyo inadhamiwa na gazeti la Raha Tele

Monday, May 14, 2012

SIMBA YATOLEWA KOMBE LA SHIRIKISHO KWA PENATI


Mabingwa wa Tanzania bara,Simba ya Dar es salaam wametolewa kwenye ya kombe la shirikisho Afrika kwa kufungwa jumla ya mabao ya 3-0 na timu ya Al-ahly shandy ya Sudan.
Al-ahly Shandy walipata mabao yao dakika ya 46,50 na 60 mpaka mpira unaisha Simba walikuwa nyuma kwa mabao 3-0,kwa matokeo hayo mshindi wa jumla ilibidi hapatikane kwa njia ya penati kutokana na Simba kushinda kwa idadi hiyo hiyo ya magoli kwenye mchezo wa kwanza jijini Dar es salaam.
Zilipigwa penati tisa tisa huku Al-ahly wakipoteza penati ya 3 iliyokolewa na mlinda mlango Juma Kaseja.Simba walipoteza penati ya 4 iliyopigwa na Patrick Mafisango.
Simba walipoteza penati ya mwisho iliyopigwa na Juma Kaseja.

Sunday, May 13, 2012

AIR TANZANIA YAPATA NDEGE MPYA


Shirika la ndege Tanzania limepata ndege mpya aina Boeing 737-500,ndege hiyo inategemea kuanza safari zake wiki ijayo kwenye miji kati ya Dar-Kilimanjaro na Mwanza.

Monday, May 07, 2012

SIMBA YAWAHARIBIA YANGA HISTORIA


Timu ya Simba jana imewafunga mahasimu wao Yanga kwa magoli 5-0 ambayo ni idadi kubwa ya magoli kwa zaidi ya miaka 37,ambapo mwaka 1976 Simba walipata ushindi wa goli 6 na kusababisha Yanga kusambaratika.
Simba walipata bao la mapema kupitia kwa Emanuel Okwi dakika ya kwanza,bao la pili dk.54 lilifungwa na Felix Sunzu kwa penati,bao la tatu dk.61 na Okwi,goli la nne 67 Kaseja kwa penati na la tano dk.72 Patrick Mafisango dk.72 kwa penati.
Baada ya mchezo huo mwalimu msaidizi wa timu hiyo ya Yanga Fred Felix Minziro Kataraiya alisema "timu ni nzuri tatizo ni migogoro iliyoko ndani ya klabu hiyo"
Nao wapenzi wa klabu hiyo wameutupia lawama uongozi wa timu hiyo kwa kushindwa kuongoza timu hiyo na kusababisha timu kuwa katika kipindi kigumu kwa msimu huu.

CHELSEA FC BINGWA WA FA CUP


Timu ya Chelsea FC imefanikiwa kutwaa ubingwa wa FA jana usiku kwa kuwafunga Liverpool 2-1 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa uwanja wa Wembly jijini London.
Chelsea walipata bao lao la kwanza kupitia kwa Lamires dk.ya 10,la pili kwa Drogba dk.59 na Liverpool likifungwa na Andy Carrol aliyeingia kipindi cha pili.


MICHEZO YA UMISETA WILAYA YA MBOZI YAFUNGULIWA LEO.


Michezo ya UMISETA kwa wilaya ya Mbozi imefunguliwa leo na afisa elimu wa wilaya hiyo kwenye viwanja vya shule ya sekondari ya Vwawa.
Michezo hiyo itazishirikisha shule za sekondari wilayani humo.

Saturday, May 05, 2012

MTIBWA YAWAPA SIMBA UBINGWA KIRAHISI.


Timu ya Mtibwa jana imewapa ubingwa Simba baada ya kuwafunga Azam bao 2-1 kwenye mchezo wa marudiano uliochezwa uwanja huru kwa timu zote,uwanja wa Taifa na kwa matokeo hayo Azam hawawezi kufikisha pointi 59 ambazo Simba wanazo tayari,huku Azam wakiwa na pointi 53 na kubakiwa na mchezo mmoja kwa kila timu.

RASHID YEKINI AFARIKI DUNIA.


Mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Nigeria na mchezaji bora wa kwanza wa Afrika mwanzoni mwa miaka ya tisini baada ya utaratibu huu kuanzishwa.
Yekini amefariki akiwa na umri wa miaka 48 na ameichechezea timu yake ya taifa kwa mafanikio makubwa kabla ya kutundika daluga.

Thursday, May 03, 2012

MZEE WAWILA HERMAN NZOWA AJITOLEA KUHAMASISHA ELIMU WILAYANI MBOZI.


Mzee Wawila Hermain Nzowa(84) mkazi wa kijiji cha Igamba wilayani Mbozi,amekuwa akipita kwenye shule za sekondari na msingi wilayani Mbozi.kuhamasisha wanafunzi kujisomea na kuepukana na maambukizi ya ukimwi.
Mzee Nzowa amesema amekuwa akifanya shughuli hii kwa kutembea shule hadi shule,mzee huyu ameomba taasisi au watu binafsi kumsaidia ili kuweza kuokoa taifa la kesho.

Sunday, April 29, 2012

SIMBA YAWATUMIA SALAMU YANGA.


Timu ya Simba ya Dar es salaam,kwa mara nyingine imeendeleza ubabe wake baada ya kuwachapa El-Ahly ya Sudan kwa mabao 3-0,kwenye mchezo wa kombe la shirikisho,uliochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Simba walipata mabao yao kupitia kwa Haruna Moshi dk.67,Patrick Mafisango dk.77 na Emanuel Okwi dk.84,kwa matokeo hayo yanaipa Simba asilimia kubwa ya kuingia robo fainali ya michuano hiyo na El-Ahly kuwa na deni la bao 4-0 kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa Sudan kati ya mei 11 au 12,baada ya kuvaana na watani wao wa jadi Yanga ambao wanaonekana kupoteana mchezo huo utachezwa mei 5 kuhitimisha ligi kuu ya Tanzania bara.

SIMBA YAWATUMIA SALAMU YANGA.


Timu ya Simba ya Dar es salaam,kwa mara nyingine imeendeleza ubabe wake baada ya kuwachapa El-Ahly ya Sudan kwa mabao 3-0,kwenye mchezo wa kombe la shirikisho,uliochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Simba walipata mabao yao kupitia kwa Haruna Moshi dk.67,Patrick Mafisango dk.77 na Emanuel Okwi dk.84,kwa matokeo hayo yanaipa Simba asilimia kubwa ya kuingia robo fainali ya michuano hiyo na El-Ahly kuwa na deni la bao 4-0 kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa Sudan kati ya mei 11 au 12,baada ya kuvaana na watani wao wa jadi Yanga ambao wanaonekana kupoteana mchezo huo utachezwa mei 5 kuhitimisha ligi kuu ya Tanzania bara.

MLIPUKO WATOKEA KANISANI NAIROBI


Waumini wa kanisa la God's House of Miracle leo asubuhi wamekumbwa na dhahama baada ya mlipuko kutokea kanisani wakati wa ibada na kuuwa mtu mmoja na wengine zaidi ya saba kujeruhiwa.
Kanisa hilo lipo maeneo ya mtaa wa Ngara,jijini Nairobi,mlipuko huo unasadikiwa ni wa guruneti ambalo bado halijajulikana limetegwa na nani?

MLIPUKO WATOKEA KANISANI NAIROBI


Waumini wa kanisa la God's House of Miracle leo asubuhi wamekumbwa na dhahama baada ya mlipuko kutokea kanisani wakati wa ibada na kuuwa mtu mmoja na wengine zaidi ya saba kujeruhiwa.
Kanisa hilo lipo maeneo ya mtaa wa Ngara,jijini Nairobi,mlipuko huo unasadikiwa ni wa guruneti ambalo bado halijajulikana limetegwa na nani?

Wednesday, April 25, 2012

CHELSEA YATINGA FAINALI KWA MGONGO WA BARCELONA.


Timu ya Chelsea imeingia fainali ya klabu bingwa ulaya baada ya kufungana FC Barcelona 2-2 kwenye uwanja wa Nou Camp kwenye mchezo wa nusu fainali.
Chelsea imefanikiwa kuingia fainali kwa jumla ya mabao 3-1,wiki mbili zilizopita ilipata ushindi wa goli 1-0 jijini London kwenye uwanja wa Stamford Bridge.
Magoli ya Barca yalifungwa na Sergio na Iniesta na Chelsea walisawazisha kupitia Lamires na Tores.

ZAO LA PARETO HATARINI KUTOWEKA


Zao la pareto ni miongoni mwa mazao ambayo wakulima wamekuwa wakiacha na kupunguza kuyalima,huenda ni kutokana na bei yake kuwa chini au soko kusumbua.
Kamera yetu ilipita maeneo ya wilaya ya Makete,kata ya Matamba na kuona zao hilo likiwa kwenye shamba la ekari moja ndani ya kijiji kizima huku kukiwa na mazao kama mahindi,ngano,maharage na alzeti kwa wingi.

Tuesday, April 24, 2012

UPONDAJI WA KOKOTO WAZIDI KUONGEZEKA MBEYA.


Kutokana na ugumu wa maisha,vijana wengi wamekuwa wakijishughulisha na kazi mbalimbali jijini Mbeya,ikiwemo kuponda kokoto pembezoni mwa barabara kuu,kamera yetu ilipita maeneo ya Ilomba jijini Mbeya na kukuta wajasiliamali wakiponda kokoto na kuuza kwa kipimo cha debe kwa sh.1500/= bila kujali jua kali lililokuwa likiwaka na kuwa kandokando ya barabara jirani na kituo cha mafuta.
Tunawaomba viongozi na taasisi mbalimbali kuweza kuwasaidia wajasiliamali hawa kuwaboreshea mazingira yao ya kazi kwa kutoa mikopo au kuwapatia vifaa vya kujikinga wanapofanya kazi zao.

Wednesday, April 18, 2012

SIMBA BINGWA KWA 92%


Timu ya Simba ya Dar es salaam leo imejiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa Tanzania bara baada ya kuwafunga JKT ruvu jumla ya mabao 3-0 kwenye uwanja wa Taifa.
Mabingwa watetezi timu ya Yanga imepoteza dira baada ya kupokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar,tunaweza kusema Yanga imevuliwa ubingwa kwani hata wakishinda mechi zao zilizobaki watafikisha pointi 52 ambazo Simba wameshavuka kwa sasa wana pointi 56 ambazo Yanga hawawezi kuzifikia.

MKUU WA WILAYA AFUNGUA KONGOMANO LA MADEREVA MBEYA.


Mkuu wa wilaya ya Mbeya,ndg Evance Balama akiongea na baadhi ya madereva wa mjini Mbeya kwenye ukumbi wa JM Hotel.
Bwana Balama aliwaasa madereva hao kujiendeleza kielimu na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

MARCIO MAXIMO AKUTANA NA MHESHIMIWA RAIS NCHINI BRAZIL

m

Aliyekuwa kocha mkuu wa Taifa stars mbrazil Marcio Maximo alikutana na mheshimiwa rais Jakaya Kikwete jijini Sao Paulo na kusalimiana naye,kabla ya kuongea na waandishi wa habari ambao walikuwa wakimuuliza kuhusu mpango wake wa kuja nchini tena kwa ajili ya kuifundisha Yanga au Azam lakini hata hivyo alikanusha uvumi huo.

Monday, April 16, 2012

MWENYEKITI WA VIJANA CCM MKOA WA ARUSHA AHAMIA CHADEMA

Mwenyekiti wa vijana wa CCM mkoa wa Arusha ameamua kujitoa kwenye chama hicho na kujiunga na Chadema,hii ni ishara ambayo si nzuri kwa chama cha mapinduzi baada ya vijana wengi kuanza kujiingiza kwenye siasa na kujiunga na kambi ya upinzani.

Sunday, April 08, 2012

TUNAWATAKIA PASAKA NJEMA.


Kwa niaba ya mtandao huu,tunawatakia wakristo na wananchi wote sikukuu njema ya Pasaka,tukiwakumbusha kutenda yaliyo mema siku zote za maisha za maisha yetu.

Saturday, April 07, 2012

STEVEN KANUMBA AFARIKI DUNIA.


Kanumba enzi za uhai wake
Msanii na mwigizaji maarufu nchini Steven Kanumba amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Kifo cha Kanumba kimewashitua watu wengi nchini na nchi jirani

SIMBA HAO 16 BORA KOMBE LA SHIRIKISHO


Timu ya Simba ya Dar es salaam jana ilifanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya kombe la shirikisho licha ya kufungwa bao 3-1 na Es Satif kwenye uwanja wa May 8 mjini Satif-Algeria.
Simba wakicheza pungufu baada ya mlinzi wake kucheza faulo ya kizembe na kutolewa kwa kadi nyekundu dk.8,walibanwa sana wapinzani wao na kujipatia magoli hayo matatu.
Simba walitulia dak 7 za mwisho na kuweza kupata goli dk.92 likiwekwa kimiani na Emanuel Okwi na kuwafanya Simba kusonga mbele kwa faida ya goli la ugenini,wiki mbili zilizopita Simba walishinda 2-0 jijini Dar es salaam.

Friday, April 06, 2012

RAIS WA MALAWI BINGU WA MUTHARIKA AFARIKA DUNIA.


Rais wa Malawi BINGU WA MUTHARIKA amefariki dunia leo hii nchini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu baada ya kupata mshituko wa moyo akiwa ofisini kwake hapo jana.
Rais Bingu wa Mutharika alizaliwa 24/02/1934 na alionyesha nia ya kuwa kiongozi toka mwanzoni mwa miaka ya 1990 na hatimaye ndoto yake ilitimia na kuwa rais wa nchi hiyo kupitia uchaguzi uliopita.
Habari hizi ni kwa hisani ya Nyasa Times.

Thursday, April 05, 2012

MHESHIMIWA LEMA AVULIWA UBUNGE ARUSHA MJINI NA MAHAKAMA

Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amevuliwa ubunge wa jimbo la Arusha mjini baada kushindwa kesi iliyokuwa inamkabili toka alipotangazwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
  Kesi hiyo ilikuwa ni ya kupinga matokeo ambayo ilifunguliwa na wapinzani wake kwenye uchaguzi uliofanyika mwaka 2010.

Wednesday, April 04, 2012

TFF YAWASHIKA YANGA PABAYA


Yanga sasa inaonekana kuchanganyikiwa baada ya kupokwa ushindi dhidi ya Coastal Union baada ya kumchezesha beki wake Nadir Haroub 'Canavaro' ambaye alikuwa ana kadi nyekundu aliyopata baada ya vurugu kwenye mchezo dhidi ya Azam na kusababisha baadhi ya wachezaji wa Yanga kufungiwa kabla ya adhabu hizo kusimamishwa na Tibaigana.

Monday, April 02, 2012

JOSHUA NASSARI MBUNGE MPYA ARUMERU KUPITIA CHADEMA.


Joshua Nassari ameibuka mshindi katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Arumeru baada kumbwaga mpinzani wake wa karibu Sioi Sumari kwa zaidi ya kura 5000.
Uchaguzi ulifanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo mh.Jeremiah Sumari wa CCM,uchaguzi huo umefanyika jana licha ya kukumbwa na matukio madogodogo ya wanachama kulinda kura na vituo vya kuhesabia kura hizo.
Baadhi ya watu wako mitaani wakishangilia ushindi huo.

Monday, March 26, 2012

MASHABIKI NDIO WANAUWA SOKA LA TANZANIA.


Katika hali isiyo ya kawaida,mashabiki wa soka hapa nchini wakifanya vitu vya tofauti sana ukilinganisha na nchi nyingine.
Haya ni moja ya matatizo ya mashabiki:-
1.Kuzomea timu ya taifa inapocheza.
2.Kuzomea baadhi ya wachezaji Taifa Stars,mfano Mwaikimba na Boko.
3.Kushangilia wageni kwenye michuano mbalimbali sababu ya Usimba na Uyanga.
4.Kutolipa viingilio vilivyopangwa.
5.Hawahudhurii kwenye mechi kama vile Villa Squad v/s Polisi Dom.
6.Kuwarushia chupa na makopo wachezaji na makocha.
7.Kutumia lugha chafu badala ya kushangilia.
8.Wanahitaji ushindi tu sio kushindwa.
9.Wanataka mafanikio ya haraka bila kujiandaa
Hizi ndizo sababu zinazoua soka la Tanzania na kuwapa wakati mgumu makocha na wachezaji wa kigeni.

SIMBA YAWACHAPA ES SATIF YA ALGERIA 2-0


Timu ya Simba leo imefanikiwa kuwafunga El Satif 2-0, kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam,mchezo huo ulikuwa ni wa kombe la shirikisho.
Simba walipata mabao hayo kipindi cha pili yakiwekwa wavuni na Moshi Kazimoto na Haruna Moshi,Simba walikianza kipindi cha pili kwa kasi na kutawala eneo la kiungo na wapinzani wao wakiwa na wakati mgumu wote wa dakika 30 za mwanzo cha kipindi cha pili.
Es Satif wakiongozwa na Yousef Satif walishindwa kuhimili muziki wa Simba kutokana na mikakati ya wachezaji wa Simba.

Tuesday, March 20, 2012

FABRICE MUAMBA SASA ANAENDELEA VIZURI


Mchezaji wa Bolton ya Uingereza Fabrice Muamba sasa anaendelea vizuri baada ya kuweza kupumua mwenyewe bila msaada wa mashine na ameweza pia kuwatambua baadhi ya watu waliomtembelea hospitali leo.
Muamba alianguka ghafla kwenye mchezo wa kombe la FA kwenye uwanja wa White hart lane,wakati timu yake ikicheza na Tottenham Hotspur,mchezo huo ilibidi huahirishwe kutokana na hali ya Muamba kuwa mbaya,huku matokeo yakiwa 1-1 na kukimbizwa hospital ya Heart attack Centre jijini London.
Muamba alijiunga na Bolton 2008 akitokea Birmingham City kwa ada ya paundi (£) milion 5.
Muamba alizaliwa DRC miaka 23 iliyopita,na alipokuwa na umri wa miaka 11 alimufuata baba yake jijini London ambako alikuwa akifanya kazi.
Tukio hili limewakumbusha wanasoka na wapenzi wa soka mchezaji wa zamani wa Cameroun Mark Vivien Foe ambaye naye alianguka uwanjani na kupoteza maisha.

KANISA KUU KATOLIKI SUMBAWANGA NI MOJA YA VIVUTIO VYA MJI HUO.


Mdau wetu akiwa nje ya kanisa kuu la katoliki Sumbawanga Mjini.
Kanisa hilo ni moja ya majengo yanayopendezesha mji huo kutokana na usafi wake.

Sunday, March 18, 2012

MAZISHI YA DIWANI WA KATA YA MYOVIZI MH.SUNDAY SHULA YAFANYIKA LEO.


Umati wa waombolezaji wakiwa kijijini Ichesa wilayani Mbozi,wakkwenye mazishi ya diwani wa kata ya Myovizi kwa tiketi ya CCM.
Mh.Shulla alifariki jana asubuhi katika hospitali ya wilaya ya Mbozi na mazishi yake ndio yanafanyika muda huu.

Saturday, March 17, 2012

UJENZI WA BARABARA KWA KIWANGO CHA LAMI WAENDELEA KWA KASI SUMBAWANGA-TUNDUMA


Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami unaendelea kwa kasi eneo la Kaengesa.
Mdau wetu alipita maeneo na kukuta kazi hiyo ikiendelea licha ya mvua nayo kuendelea kunyesha.

Friday, March 16, 2012

AFRICAN RAINBOW SECONDARY YACHAPWA NA MAZWI SECONDARY KWENYE MCHEZO WA KIRAFIKI.


Timu ya netball ya Mazwi Secondary leo imewafunga wenzao wa African Rainbow mabao 46-39.
Nyota wa mchezo wa leo alikuwa Georgina Maheka wa Mazwi licha ya kukabiliana na ukuta mgumu wa African Rainbow ukiongozwa na Tamali Joseph.
Mchezo umechezwa kwenye uwanja wa Mazwi Secondary.

Thursday, March 15, 2012

LIGI YA MKOA WA RUKWA JAMAICA YAIFUNGA RUKWA UNITED 2-1


Timu ya Jamaica FC imeifunga timu ya Rukwa united bao 2-1,kwenye ligi ya mkoa huo,magoli ya Jamaica yamefungwa na Steve Mwansite dakika ya 4 na la pili likifungwa na Torres,bao la kufutia machozi la Rukwa united limefungwa kwa njia ya Penati.

Monday, February 13, 2012

ZAMBIA MABINGWA WA AFRIKA 2012


Timu ya taifa ya Zambia(Chipolopolo) imefanikiwa kutwaa kombe la mataifa ya Africa usiku baada ya kuwashinda Ivory Coast kwa mikwaju ya penati 8-7.
Timu hizo zilicheza kwa dakika 120 na matokeo kuwa 0-0 na hivyo kuingia kwenye matuta ambapo kila ilipiga penati 9,Zambia ilikosa moja na Ivory Coast ilipoteza 2.
Shukrani za pekee zimuendee golikipa wa Zambia Kenedy Mwene, ambaye alikuwa nyota wa mchezo kwa dakika zote na kuweza kuokoa penati 1 kutokana na umahiri wake.

Sunday, February 12, 2012

WHITNEY HOUSTON AFARIKI


Mwanamuziki maarufu nchini Marekani amefariki usiku wa jana,mwanadada huyo ambaye alikuwa akihusishwa na utumiaji wa madawa ya kulevya lakini aligeuka na kuanza kupinga utumiaji wa madawa hayo kwa watu wengine.
Mwanadada amekuwa na sifa za uvumilivu kwenye mahusiano yake ya kimapenzi licha ya kupitia mikasa mbalimbali lakini aliweza kuvumilia pamoja na umilionea aliyokuwa nao.

Thursday, February 09, 2012

TIMU YA TAIFA YA ZAMBIA YAINGIA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA.


Timu ya taifa ya Zambia (Chipolopolo) imefanikiwa kuingia fainali ya michuano ya mataifa ya Afrika, baada ya kuwafunga Ghana(Black Star) kwa bao 1-0,
Zambia walipata bao lao kupitia kwa kupitia kwa Emanuel Mayuka dakika ya 78 na kuwafanya Zambia kuingia fainali,katika mchezo mwingine wa nusu fainali Ivory Coast wameifunga Mali bao 1-0.
Sasa Zambia watakutana na Ivory Coast katika mchezo wa fainali utakaochezwa kesho kutwa na Ghana watawakabili Mali katika kuwania nafasi ya tatu.

Wednesday, February 08, 2012

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

Wednesday, February 01, 2012

MVUA NI NEEMA TATIZO SISI


Kutokana ni miundo mbinu mibovu mvua imekuwa kama kero kwa wakazi wa Soweto jijini Mbeya,wamekuwa wakipata taabu kwenye maeneo ya barabara zinazoingia na kutoka mitaa hiyo kutokana na maji kujaa na kuhathiri mpaka maeneo ya biashara.kama inavyoonekana kwenye picha.

MTI HUU UNAWEZA UKASABABISHA AJALI.


Mti huu matawi yake yameingia barabarani na kusababisha mtu unayetembea kwa miguu usiweze kuliona gari linalokuja mbele au nyuma kutokana na matawi yaliyozidi na kuingia mpaka barabarani kwenye barabara ya Uhindini kuelekea Soko matola jijini Mbeya,wahusika inabidi walishughulikie suala hili mapema kabla madhara hayajatokea.

JIJI LETU MBEYA LEO


Picha hii ni moja ya mitaa ya jiji la Mbeya.

Tuesday, January 17, 2012

WAKULIMA HAWA WANAHITAJI MSAADA WA SOKO LA BIDHAA ZAO

 Wakina mama wa kijiji cha Mshewe Mbalizi wilaya ya Mbeya vijijini wakiuza maembe kwa bei ya shilingi 500/= kwenye plastiki,ambayo ni bei isiyoendana na wingi wa bidhaa hiyo,tunawaomba wale wote wenye uwezo wa kujua soko liliko wawasaidie wakulima
 Wakina mama wakiwa na watoto wao wakisubiri wateja wa maembe kijiji hapa kama walivyokutwa na kamera yetu.

Hili ni ambalo wakina mama hawa huuzia biashara zao za matunda

Moja ya matunda yaliyopo mashambani yakisubiriwa kuvunwa matunda yanajulikana kama maparachichi au matakapela pia yanapatikana kwenye kijiji hiki.